Wanachama wa CCM,wa kata ya Makurumla,  wakisafisha makaburi ya Mburahati Dar es Salaam katika maadhimisho ya wiki ya mazingira

FARAJA MASINDE

-DAR ES SALAAM

WAKATI Wiki ya mazingira duniani ikifikia ukingoni Umoja wa Wazazi wa Chama Cha Mapinduzi(CCM), Kata ya Magomeni Makurumla umetumia wiki hiyo kuwakumbuka waliotangulia mbele za haki kwa kusafisha makaburi.

Akizungumza na leo wakati wa zoezi hilo, Katibu wa Siasa na Uenezi wa Kata ya Magomeni Makurumla, Shukuru Abdalla amesema lengo la kusafisha makaburi hayo ya Mburahati nikutokana na umuhimu wake pamoja na ukaribu wa kituo cha Afya kilichopo hapo.

Amesema zoezi hilo halitaishia leo badala yake litakuwa endelevu katika kuhakikisha kuwa makaburi hayo yanasafishwa na kuwa salama.

“Tumekuja katika eneo hili la makaburi sababu tuko kwenye maadhimisho ya wiki ya mazingira duniani na sisi tumeamua kutumia siku hii kwa kufyeka na kufanya usafi katika makaburi yetu ya Mburahati kwani sisi sote tunajua ni wafu watarajiwa na hapo walipolala Wazee wetu, Mama zetu, Dada zetu na Kaka zetu ndipo tumeona ni sehemu muhimu ya kufanyia usafi kwasababu hili ni eneo muhimu sana.

“Ukiondoa eneo la makaburi, hapa pia kuna kituo cha Afya cha Makurumla hivyo majani yakiwa mengi yanaweza kuogopesha hata Manesi na Mdaktari kufika kazini hasa nyakati za usiku sababu yanaweza kuficha vibaka na watu wasiokuwa na nia njema,” amesema Abdallah.

Amefafanua kuwa, hiyo imekuwa ni kawaida ya Umoja huo katika kufanya usafi kwenye wiki ya mazingira duniani ambapo wamekuwa kifanya usafi katika kituo cha Afya, huku akisisitiza kuwa wanampango wa kuwaarifu wananchi wote kushiriki kwenye usafi wa makaburi hayo.

Aidha, ametoa wito kwa wananchi kuendelea kukiunga mkono chama cha mapinduzi kwa kuwa mietekeleza mambo mengi makubwa ndani ya miaka mitano chini ya Rais Dk. John Magufuli.

“Wito wangu kwa Watanzania huu ni mwaka wa uchaguzi hivyo wampigie kura Rais Magufuli kwani mengi tumeyaona, sasahivi hata ukitoka mkoani ukifika Ubungo pale utaona mambadiliko makubwa ukiondoa hilo ameongeza dawa katika vituo vya afya na hospitali bado anajenga mradi wa bwawa la kufua umeme la Nyerere litakalopunguza gharama za umeme kwa wananchi na mambo mengine mengi,” amese Abdalla.

Upande wake Diwani wa Viti Maalum Halmashauri ya Ubungo, kutoka Kata ya Makurumla, Rehema Mayunga, amesema wamechagua kufanya usafi wa makaburi hayo kwa kuwa ndiyo sehemu wanayoishi na kwamba wananchi wengi wamekuwa kihifadhiwa katika eneo hilo huku akimshukuru Rais Magufuli kwa namna alivyopambana na janga la corona.

“Tumefanya hivi kuwakumbuka wapendwa wetu katika kuhakikisha kuwa wanalala sehemu nzuri ikizingatiwa kuwa hii ni wiki ya mazingira. Pia niwatake wananchi hususan wanawake wenzangu kuchagua viongozi wanaoweza kuwaletea maendeleo ikiwa ni pamoja na kutatu changamoto zao, mfano mzuri ni Rais wetu ambaye nibayana kwamba ameweza kutuvusha katika mambo mengi ikiwamo janga la corona,” amesema Rehema.

Naye Katibu wa CCM kata ya Makurumla, Salama Mlaponi, amefafanua kuwa, wamechagua kufanya usafi kwenye eneo hilo la makaburi kwa kuwa wote ni marehemu watarajiwa ikiwamo kuweka mazingira safi.

“Hapa pia kuna kituo chetu cha afya hivyo tuliona ni jambo la busara kuweka mazingira mazuri hapa kwani kichaka hiki likuwa kikitishia usalama, sababu iliwahi kukutwa maiti ya kijana hivyo tunaona ni jambo la busara kuweka mazingira safi.

“Pia kuelekea katika uchaguzi mkuu Oktoba mwaka huu ushindi kwa CCM Kata ya Makurumla ni lazima na tumejipanga vyema kwenye hilo kuhakikisha kuwa kata hii inakuwa chini ya CCM,” amesema Salama.

Akizungumzia zoezi hilo, Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Kwajongo, Omar Omary amesema Jumuiya hiyo ya Wazazi imeamua kufanya hivyo ili kuweka salama makazi ya wapendwa wao na kupata fadhila za Mwenyezi Mungu.

“Nahimiza pia jumuiya nyingine kuiga utaratibu huu ikiwamo Umoja wa Vijana, Umoja wa Wanawake kuendeleza msukumo huu wa kuhudumia jamii,” amebainisha Omary.
Share To:

TANGA RAHA BLOG

Post A Comment: