Serikali Wilayani Hai imekagua ujenzi wa ukuta wa TANESCO ambapo ujenzi haukufanyika kwa zaidi ya miezi saba na kupelekea Mkuu wa wilaya hiyo Lengai Ole Sabaya kuamuru Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa TAKUKURU kuwakamata Maofisa watano wa Shirika hilo.

Ujenzi huo umeanza wiki mbili zilizopita na hadi sasa umefikia Asilimia 87 Huku DC Sabaya akitoa maelekezo kuwa kuanzia sasa TAKUKURU washiriki kuanzia hatua za awali za mradi wowote ili kuzuia ubabaishaji na uzembe wa makusudi na kuwakosea wananchi
Share To:

Post A Comment: