Ongezeko la kutelekeza watoto
wenye umri chini ya miaka saba limezidi kuchukua sura mpya
katika mkoa Tanga ambapo takwimu zinaonyesha
kutoka mashauri 115 kwa mwaka 2017/2018 hadi kufikia
387 kwa mwaka 2018/ 2019.
Kwa mujibu wa Ofisa Ustawi wa
Jamii Mkoa wa Tanga Mmasa Malugu alisema ongezeko
hilo limeendelea kushamili kutokana na sababu
mbalimbali kitu ambacho kinapelekea watoto hao
kukosa ulinzi na usalama katika makuzi yao
.
Taarifa hizo zimeendelea kuonyesha kuwa mwaka
2016 / 2017 walipokea dawatini kwao mashauri 262 kati
ya kesi hizo 49 zilipelekwa mahakanii .
Ofisa Ustawi huyo amesema
kuwa vitendo vya kutelekeza watoto ni miongoni
mwa unyanyasaji wa kijinsia ambao wanafanyiwa watoto
wenye umri huo wa chini ya miaka saba jambo
ambalo kwa asilimia kubwa watoto hao wanakosa malezi ya
baba na mama.
Alieleza kuwa baada ya kuona
tatizo hilo linazidi kushamiri, Mkoa umeamua kujikita katika
kuhakikisha miongozo inayotolewa na serikali kuhusu malezi inafuatwa kama
kuanzisha kamati za MTAKUWA ambazo zinakuwa ngazi ya vijiji ,
mtaa , kata halmshauri na Mkoa, kwa ujumla.
Mulugu Alisema kuwa lengo la
kuanzisha kamati hizo ni kutaka kusaidia katika malezi,
makuzi pamoja na kuhakikisha manyanyaso kwa watoto
yanapungua kwa kiasi kikubwa katika maeneo ambayo zipo kamati
hizo. Aliongeza kuwa kamati hizo ni mchanganyiko wa
watalaam mbalimbali na jamii ambao wanakuwa pamoja .
Ingawa haijaelezwa Kwa ni wilaya gani
inayoongoza kwa matukio kama vile ya unyanyasaji, ukatili wa
kimwili, kingono na kihisia. “Kiukweli, kesi nyingi
tulizonazo zinatokea katika maeneo ya Pwani kama vile Mkinga
, Pangani na katika shule zilizopo ndani ndani na hii inatokana na
mifumo tuliyonayo sasa,” alieleza Malugu.
Hata hivyo kuetelekeza ni pamoja na
kutotoa matumizi kama chakula, mavazi , matibabu, makazi,
na mahitaji ya msingi kama ada za shule,
vifaa vya shule na kila kitu ambacho
ni mahitaji ya msingi kwa makuzi na ustawi
wa mtoto.
Akitoa Takwimu kwenye kongamano la wadau wa ukatili dhidi ya
watoto lililofanyika Mkoani Tanga hivi karibuni , Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo
ya Watoto katika Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii ,Jinsia Wazee na
Watoto Mwajuma Magwiza, alisema takwimu za jeshi la Polisi mwaka
2018 zinaonyesha kuwa mkoa wa Tanga unaongoza kwa kuwa na visa 1039. Mkoa
wa Mbeya unashika nafasi ya pili kwakuwa na visa 1017 .
Prisca Mwakasindile, ambaye ni Muuguzi
katika kituo cha kulelea watoto wenye ulemavu kilichopo Jijini
Tanga cha YDCP amesema kuwa wamekuwa wakikutana na
changamoto mbalimbali za watoto wenye ulemavu
kutelekezwa na baba zao kutokana na hali zao .
Martin Mhina Mkazi wa Korogwe
amesema kuwa jambo la kutelekeza watoto si jambo
jema na hiyo inasabishwa na wazazi kukwepa majukumu yao
pamoja na malezi yao wenyewe. Alisema kuna wanaume
wamejipa majukumu ya kutafuta watoto lakini bado wao wanakula
kwa wazazi wao.
Mzazi mwingine
alijitambulisha kwajina la Dege Masoli mkazi wa songe kilindi
amesema kuwa sababu inayosababisha watoto
kutelekezwa inatokana na migogoro ya kifamilia , kukosekana
kwa uaminifu katika mahusiano na hali ngumu za kiuchumi
.
Mwisho..Habari na Rais Saidi Tanga
Post A Comment: