Baba Mzazi wa Marehemu Steven Kanumba, Charles Kanumba amefariki leo Machi 8, 2020, saa nne asubuhi akiwa Hospitali ya Mkoa wa Shinyanga. Mdogo wake Kanumba, Mjanaeli Kanumba amethibitisha. 

Mzee Kanumba kwa muda mrefu alikuwa anasumbuliwa na tatizo la nyonga lililosambabishwa kushindwa kutembea kwa muda mrefu na uvimbe katika kibofu cha mkojo pamoja na shinikizo la damu.

Amesema msiba upo nyumbani kwa baba huyo  Ngokolo mkoani Shinyanga na utaratibu wa ratiba za mazishi bado zinaelendea.
Share To:

msumbanews

Post A Comment: