Waratibu wa Safari hiyo kutoka nchi za Zimbabwe,Tazania na Uganda wamesema kuwa ziara hiyo inalenga kuhamasisha utalii wa ndani katika nchi za Afrika na kuwataka Vijana kujitokeza kwa wingi katika kuungana na vijana wa Afrika kupanda mlima huo unaongoza kwa urefu barani Afrika na wa pili kwa dunia nzima.
Emanuel Motta ni mratibu kutoka nchini Tanzania anasema kuwa maadhimisho ya umoja wa Afrika May 25 mwaka 2020 yatafanyika katika kilele cha mlima Kilimanjaro ambapo vijana watapeleka agenda 2063 za Afrika tunayoitaka pamoja na Malengo Endelevu ya Umoja wa Mataifa
Mdau wa Masuala ya Vijana kutoka nchini Uganda, Ayaa Musuya amesema kuwa kabla ya kupanda mlima huo kutakua na mashindano ya sanaa ya kuchora Afrika tunayoitaka na washindi watapata nafasi ya kupanda mlima huo na kupeleka sanaa zao kileleni.
Kwa upande wake mratibu wa Ziara hiyo kutoka nchini Zimbabwe Munyaradzi Muzenda amesema kuwa watakuwa na mabango makubwa ya Afrika Tunaoitaka pamoja na Agenda 2063 ya Afrika tunayoitaka ambayo yatabebwa na vijana ikiwa ni pamoja na kuhamasisha vijana kutimiza ndoto zao
Post A Comment: