Mkurugenzi wa R.D.O Fidelis Filipatali akionyesha mfano wa miradi ya maji inayotekelezwa na taasisi yake
Mkurugenzi wa R.D.O Fidelis Filipatali akizungumza na wanahabari juu ya kazi zinazofanywa na R.D.O
Filipatali wa nne kulia akiwa na washiriki wa mdahalo wa amani na uzalendo baada ya kuwakilisha taarifa ya kazi za R.D.O
Filipatali akipongezwa na Afisa wa polisi jamii mkoa wa Iringa Vicent Msami
Katika kuunga mkono jitihada za serikali ya awamu ya tano chini ya Rais Dkt John Magufuli kusogeza huduma ya maji safi na salama kwa wananchi vijijni ,asasi isiyo ya kiserikali ya Rural Development Organization -(RDO) imetumia zaidi ya shilingi bioni 1.4 kupeleka huduma ya maji safi na salama kwenye kata na vijiji zaidi ya 17 vya pembezoni mwa wilaya ya Mufindi na Kilolo mkoani Iringa .
Mkurugenzi mtendaji wa RDO ,Fidelis Filipatali alisema juzi wakati mdahalo wa kudumisha amani na uzalendo ulioandaliwa na mwamvuli wa asasi zisiyo ya kiserikali wa Iringa civil society organization( ICISO -Umbrella) kwa ajili ya kundi la wanawake ,vijana,asasi za kiaria pamoja na viongozi wa dini na vyama vya siasa mdahalo uliofanyika mjini Mafinga katika ukumbi wa shule ya Southern Highlands Mafinga .
" Sisi kama RDO tunaisaidia serikali katika mambo mbali mbali yakiwemo ya kudumisha amani katika maeneo yetu tunayofanyia kazi kuona wananchi wake wanafanya kazi kwa amani na utulivu ila pamoja na kudumisha amani tumekuwa tukiungana na serikali katika kupeleka huduma ya maji kwa wananchi ambao walikuwa hawana huduma hiyo katika wilaya ya Mufindi na Kilolo hasa vijijini " alisema Filipatali
Tumekuwa tukijikita zaidi kuwawezesha vijana kupata elimu ya uzalendo na amani kwa kuwawekea misingi mizuri ya kuja kujiajiri wenyewe kama kuwapa elimu ya ufundi kwa wale ambao walikuwa na ndoto za kukimbilia mijini pamoja na kuwapa nafasi ya kufanya kazi katika miradi ya maji .
Kuwa hadi sasa vijana wengi wame wameweza kuonyesha uzalendo wao kwa kubaki vijijini na kushirikiana na wananchi kushiriki katika ujenzi wa miradi ya maji vijijini ambapo hadi sasa vijiji takribani 17 na vituo vya kuchotea maji 230 vimepata kujengwa katika wilaya za Mufindi na Kilolo .
Wakati jumla ya watumia maji 8500 wamekwisha nufaika na mradi huo wa maji wa RDO katika wilaya ya Kilolo na Mufindi ambao wanufaika hao ni wale ambao walikuwa awali wakitumia maji ya mito yasiyo safi na salama ila sasa wanapata maji ya bomba ambayo ni safi na salama kama ilivyo kwa wananchi wa mijini.
" Kwa kufanikisha huduma hii ya maji kufika vijijini wananchi watakuwa na imani kubwa na serikali lakini pia wataweza kupata ajira zaidi kwani wanaweza kutumia muda wao kufanya shughuli za kimaendeleo badala ya kupoteza muda kwenda kutafuta maji tambua huduma zote muhimu kama maji zikipatikana vijijini vijana wanapenda vijiji vyao na Taifa na kuacha kukimbilia mijini na huo ni mwanzo wa uzalendo ndio maana falsafa ya RDO sisi ni vijijini zaidi "
Alisema kuwa miradi yao imekuwa ikipewa nguvu zaidi na kikundi kidogo cha wakulima kutoka Ulaya ambao wameweza kujibana wao na familia zao ili kusaidia watanzania wa wilaya ya Kilolo na Mufindi kuweza kupata huduma ya maji safi na salama pamoja na kuwawezesha vijana kupata elimu ya ufundi kupitia chuo cha ufundi stadi cha RDO Mdabulo na RDO Kilolo .
Hata hivyo alisema kuwa taasisi hiyo imeamua kuunga mkono jitihada zinazofanywa na serikali kwa kuwahudumia wananchi katika kuboresha sekta ya maji na elimu ya ufundi kwa kuendelea kusongeza huduma ya maji kwa wananchi wa pembezoni ambao hawakuwa na huduma hiyo .
Kuwa RDO wamefanikiwa kwa kiasi kikubwa kushirikiana na Halmashauri ya wilaya ya Mufindi katika uendelezaji wa upanuzi wa miradi ya maji safi na salama katika kijiji cha Nandala na vijiji vingine vya wilaya ya Mufindi kama Mpanga Tazara ambako ni pembezoni kabisa mwa mwilaya ya Mufindi pamoja na vijiji vya wilaya ya Kilolo .
Filipatali alisema shughuli za usimamizi wa miradi hiyo zimekuwa zikifanywa kwa ushirikiano mkubwa wa serikali za vijiji husika na miradi hiyo husimamiwa na wananchi wenyewe kupitia jumuiya za watumiaji maji japo changamoto zinazokabili miradi hiyo kuwa ni kutowajibika ipasavyo kwa baadhi ya watumiaji maji kutotimiza wajibu wao pamoja na baadhi ya wanasiasa kutumia miradi hiyo kujitafutia umaarufu wa kisiasa .
Alisema RDO imejipanga kuendeleza upanuzi wa miradi ya maji katika vijiji ambavyo vina changamoto ya maji baadhi ya vitongoji ambavyo vilikuwa havina huduma ya maji kwenye wilaya ya Mufindi na Kilolo lengo likiwa ni kuweza kuwafikia wananchi wenye uhitaji wa huduma hiyo .
Post A Comment: