NA HERI SHAABAN
MBUNGE wa Segerea Bonah Ladislaus ameunda  Kamati Maalum   Wananchi wa Kata ya Kinyerezi Manispaa ya Ilala  kwenda kuonana na Mkurugenzi wa Kampuni ya Reli TRL kwa ajili ya fidia kupisha mradi wa Reli ya kisasa ambao umepita Mtaa wa Kifuru.


Kamati hiyo ilichaguliwa  ya watu kumi Leo katika mkutano wa hadhara  ulioandaliwa na Mbunge wa Segerea Bonah Ladslaus ulifanyika eneo la Kifuru Wilayani Ilala kwa ajili ya kusikiliza kero za wananchi  .


Akizungumza katika kikao hicho Bonah alisema  dhumuni la mkutano huo kusikiliza kero za wananchi  kuzifanyia kazi na  kuelezea mafanikio ya miaka minne akiwa Mbunge wa Segerea yale aliotekeleza kwa wananchi.

Bonah alisema ziara  hiyo ni endelevu anaongozana na Wataalam mbalimbali  wakiwemo DAWASA   kwa  ajili ya kusikiliza matatizo ya wananchi katika maeneo yenye changamoto ya Maji.

" Kata ya Kinyerezi umepita mradi wa Reli ya kisasa kuhusiana na suala la Fidia naomba tuchague Kamati maalum jumatatu tutaongozana kumuona  mkurugenzi Mkuu wa Reli  MHANDISI Kadogosa kujua malipo yenu mtalipwa lini ili kupisha mradi wa Serikali hivyo naomba msiwe na wasiwasi  Serikali hii ni sikivu" alisema Bonah.

Bonah ameunda Kamati hiyo kufuatia wananchi zaidi ya 100 wapo njia panda wakisubili fidia kupisha mradi huo wa Reli ya Umeme.

Wakati huo huo ameunda Kamati ya kufatilia mradi wa Maji katika mtaa wa Kifuru ambapo Maji hayo yanatarajia kufika February mwaka 2020   .

Akielezea mafanikio yake kwa Kata ya Kinyerezi katika kuisaidia Serikali ya Rais John Magufuli sekta ya elimu ametoa fedha za jimbo la Segerea shilingi million 50 zimejenga madarasa sita pia fedha nyingine zimeweka umeme Shule ya MSINGI Zimbili na sasa wanafunzi wanasoma mazingira ya shule hizo yapo vizuri .

Pia aliezea mafanikio mengine alisema jimbo la Segerea kwa sasa Maji yapo kwa asilimia 90  maeneo yaliokosa Maji yatafika kwa wakati awali wakati anaingia madarakani mwaka 2015  maeneo mengi Maji yalikuwa hayajafika kwa sasa Maji yamefika kwa asilimia 90 .

Aliwataka Wanawake na Vijana waunde vikundi mbali mbali kwa ajili ya Mikopo ya Serikali ambayo inatolewa na Halmashauri ya Ilala aina riba kila kikundi kiandae Katiba washirikiane na Mama Maendeleo wa Kata watapewa taratibu za usajili.

Akielezea kuhusu Barabara za Mtaa alisema ameshazungumza na Mhandisi wa Tarura kuanzia Jumatatu barabara za Mtaa zote zitakarabatiwa.


Kwa upande wake Mhandisi wa DAWASA Tabata Julias Kulwa alisema  Kata ya Kinyerezi Mtaa wa Kifuru watapata maji ya DAWASA kutokeq Kimara kwa sasa Maji yapo njiani na katika mikakati ya mwisho Mali ghafi za mradi huo zimekamilika iifikapo February 2020 wananchi wote watapata Maji.

Naye Polisi Kata Kinyerezi Peter Lusinde aliwataka waunde Polisi Jamii ili washirikiane na Jeshi la Polisi ili Kinyerezi iwe Salama katika kukomesha wahalifu.


Mwisho.
Share To:

msumbanews

Post A Comment: