Viongozi wa ICISO ,jeshi la polisi na MNGONET wakiwa katika picha ya pamoja na kundi la wanawake walioshiriki mdahalo wa amani ,uzalendo
Kundi la vijana katika picha ya pamoja
Washiriki wakiwa katika mdahalo
Mwenyekiti wa MUNGONET Boniface Mlinga akitoa vitambulisho
Mtendaji mkuu wa ICISO Raphae Mtitu akitoa elimu
ASASI isiyo ya kiserikali ya Iringa society Organization (ICISO) kwa kushirikiana na USHIRIKI TANZANIA chini ya imeanza kuendesha midahalo kuwaandaa watanzania katika ushiriki wa uchaguzi mkuu mwaka 2020 kwa amani na uzalendo pasipo kujiingiza katika machafuko .
Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mdahalo ulioshirikisha vijana ,wanawake na viongozi wa taasisi za dini na vyama vya siasa jana katika ukumbi wa Southern Highlands mjini Mafinga mtendaji mkuu wa ICISO Raphael Mtitu alisema kuwa asasi yake ni miongoni mwa asasi 23 Tanzania zinazowezeshwa na USHIRIKI TANZANIA katika kutoa elimu kwa watanzania juu ya elimu ya amani ,uzalendo na ushirikishwaji .
Mtitu alisema kuwa katika midahalo hiyo wamekuwa wakizingatia mambo ya msingi kwa ajili ya kuwaandaa watanzania kushiriki kwa amani na utulivu katika uchaguzi mkuu na kuwa ushiriki Tanzania ni mtandao ambao unaunganisha pamoja asasi 23 za kiraia zinazolenga kujenga demokrasia na utawala bora kwa vijana ,wanawake ,na wenye ulemavu kwa kuwajengea uwezo kupitia tafiti na mitandao ya kijamii .
Aliema kuwa kupitia midahalo hiyo ambayo inafanyika katika wilaya zote za mkoa wa Iringa kwa makundi lengwa zitasaidia kukuza ushiriki wa wanawake ,vijana na wenye ulemavu kufanya mazungumzo na kushirikiana na serikali ya Tanzania katika maamuzi na utungaji wa ser hususani katika masuala ya muungano .
Pia kutetea sera shirikishi kwa wanawake ,vijana na wenye ulemavu katika mchakato wa uchaguzi kutoa taarifa kwa umma kuhusu masuala yanayohusu wanawake vijana na wenye ulemavu ,nafasi ya raia na mchakato wa uchaguzi .
Mtitu alisema kuwa kupitia midahalo hiyo na elimu wanayoitoa wataweza kuhamasisha vijana ,walemavu na wanawake kujitokeza kwa wingi katika ushiriki wa uchaguzi mkuu na pamoja na kujitokeza kugombea nafasi mbali mbali .
Wakichangia mada katika mdahalo huo viongozi wa taasisi za dini mchungaji wa kanisa la kiinjili la kilutheri Tanzania (KKKT ) mtaa wa Isalavanu Bahati Kitinusa alisema kuwa wao kama kanisa wamekuwa wakitoa elimu kwa waumini wao namna gani ya kuishi kwa uzalendo na kudumisha amani kupitia ibada zao .
Alisema kuwa mdahalo huo umekuja wakati sahihi kwa jamii ya wilaya ya Mufindi kujiandaa kudumisha amani wakati wa kuelekea katika uchaguzi mkuu mwakani ambapo kila mmoja analo jukumu la kuenzi amani na uzalendo wa Taifa badala ya kukubali kutumiwa nawasio penda amani hii.
Huku mchungaji wa Kanisa la Triity Ostari Mafinga Amani Kiwale alisema kuwa dini ni nzuri sana na viongozi wa dini ni wazuri ila iwapo watatumia vibaya midomo yao na majukwaa ya dini ni hatari sana kwa ustawi wa Taifa na hivyo lazima kwa viongozi wa dini kuwa mfano mwema wakulinda ndimi zao wakati wote .
Pia alisema kwa viongozi wa siasa nao wanajukumu la kudumisha amani na utulivu wa nchi kwa kutumia vema nafasi zao na kuepuka kauli zenye vikwazo ambazo zinaweza kuligawa Taifa .
Huku vijana na wanawake waliopata kushiriki mdahalo huo wakichangia mada katika mdahalo mbali ya kuponbeza asasi ya ICISO kwa kuwafikia vijana hao kupitia mdahalo huo bado waliomba elimu hiyo kuendelea kutolewa Zaidi hasa kwa kuelekeza vijijini Zaidi ambapo wengi hawajui chochote .
Kwa upande wake mkurugenzi wa Rural Development Organization (RDO) Fidelis Filipatali alisema kuwa suala la amani na uzalendo limekuwa likianza kwa kuwaandaa vijana kuwa wazalendo kwa kuwapatia elimu ya ufundi bure pamoja pamoja na elimu ya kujiandaa kimaisha .
Kwa upande wake katibu wa mtandao wa muungano wa asasi za kiraia wilaya ya Mufindi ( MUNGONET) Renatus Mpiluka ambao pia ni washiriki wa mdahalo huo wakijibu swali la vijana juu ya asasi kwenda vijijini kutoa elimu kwa vijana na walemavu alisema kuwa asasi yake na nyingine wamekuwa wakitoa elimu katika maeneo mbali mbali ya wilaya hiyo alisema wao pamoja na asasi za kiraia wilaya hiyo wamejipanga kutoa elimu ya uraia kwa mpigakura ili kujua wajibu wao kuanzia wakati wa kujiandikisha ,kampeni ,kupiga kura na kuepuka kushiriki vitendo vyovyote vya uvunjifu wa amani
Post A Comment: