Kaimu Mganga Mkuu wa Hospitali ya Mkoa wa Singida, Ernest Mugetta, akizungumza kwenye kikao cha tathmini ya ugonjwa wa Trakoma cha robo  tatu ya nne ya mwaka kilicho wakutanisha wadau wa Sekta ya Afya kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Itigi na Manyoni mkoani Singida jana.
 Afisa Mradi wa Trakoma  kutoka Shirika la Helen Keller International, Athuma Tawakal, akizungumza na waandishi wa habari kwenye kikao hicho kuhusu ugonjwa huo.
 Washiriki wa kikao hicho wakiwa kwenye majadiliano.
 Dkt. Peter Kabangila (kushoto) kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Itigi, akijadiliana jambo na Mratibu wa Huduma za Macho Wilaya ya Ikungi, Shija Mhoja katika kikao hicho.
 Majadiliano yakiendelea. Kutoka kushoto ni Kaimu Mratibu wa Huduma za Macho Wilaya ya Manyoni, Renatus Ngeze, TT Surgeon Wilaya ya Manyoni, Bukumbi Makoye na Mratibu wa Magonjwa yaliyokuwa hayapewi Kipaumbele (DNTDCO) Wilaya ya Mkalama DC, Dkt. Julius Nyenje.
 Kikao kikiendelea.
 Kikao kikiendelea.
Kikao kikiendelea.
Kikao kikiendelea.
Na Waandishi Wetu, Singida
CHANGAMOTO ya uhaba wa maji na usafi wa mazingira vimetajwa kuwa miongoni mwa sababu zinazopelekea  kushamiri kwa ugonjwa wa Trakoma  kwenye baadhi ya halmashauri za mkoa wa Singida, zikiwemo Manyoni na Itigi  imeelezwa.  
Trakoma ni ugonjwa unaoathiri macho ambapo kope huingia ndani na kugusa jicho hatimaye matokeo ya hali hiyo huweza kusababisha mtu kutoona vizuri au kuwa kipofu.
Akizungumza na waandishi wa habari kwenye kikao cha tathmini ya robo mwaka, kilichowakutanisha wadau mbalilmbali wanaojihusisha kukabiliana na ugonjwa wa Trakoma ndani ya halmashauri za wilaya ya Manyoni na Ikungi mkoani hapa jana, Kaimu Mganga Mkuu wa Hospitali ya Mkoa wa Singida, Dkt. Ernest Mugetta, alisema pamoja na dalili za mafanikio zilizopo lakini bado kuna jitihada za ziada zinahitajika kwa kila mdau katika kutokomeza kabisa ugonjwa huo.  
”Tunaendelea kutoa elimu hususan kwenye kuzingatia usafi wa macho, maji na kunawa uso vizuri…hivi ni vitu ambavyo tunaendelea kuvisisitiza sana kwenye jamii ili kupunguza  trakoma,”  alisema Dkt. Mugetta na kubainisha kuwa sehemu kubwa ya jamii inayoathirika na ugonjwa  huu ni ile ambayo upatikanaji wake wa maji ni mdogo. 
Alisema serikali  kwa kushirikiana na Shirika lisilo la kiserikali la Helen Keller International kwa mda mrefu sasa wameendelea kutoa huduma za afya ya macho kwa mafanikio ndani ya Halmashauri za Manyoni na Itigi na kuhamasisha umma juu ya kuchukua tahadhari, ikiwemo kuzingatia usafi wa macho wakati wote katika kukabiliana na ugonjwa huo hatari unaowakumba watu wote wenye umri wa miaka 15 na kuendelea.   
Kikao cha wadau hao, pamoja na mambo mengine kilipitia taarifa za halmashauri zilizofikiwa na mradi huo sanjari na kujadili mwelekeo wa kuingiza halmashauri nyingine zenye changamoto ya ugonjwa huo kwa utekelezaji wa mradi.   
Afisa Mradi wa Trakoma kutoka Shirika la Helen Keller International, Athuman Tawakal, alisema tatizo lipo kwa mda mrefu lakini limekuwa likipungua kadri siku zinavyokwenda.   
“Juhudi kubwa iliyopo kwa sasa ni kuhamasisha jamii kuondokana na visababishi vyote vinavyoweza kusababisha ugonjwa huu ikiwemo kuzingatia suala la usafi wa mazingira, upatikanaji wa maji ya kutosha ndani ya jamii, ujenzi wa vyoo bora na kutoa matibabu kwa wale wote ambao wameathirika dhidi ya Trakoma
Share To:

msumbanews

Post A Comment: