Kabla ya kuangalia namna ya kujitoa kwenye huduma hii, kwanza ningependa tuanze kwa kutoa ufafanuzi Truecaller ni nini?

TrueCaller ni app maarufu duniani inayowawezesha watumiaji wake kutambua majina ya watu au makampuni wanayotaka kuwasiliana nayo au yanayowapigia simu wao.

Kwa kifupi, mtumiaji wa TrueCaller anaweza kufahamu jina la mtu au kampuni  hata kama hajam save kwenye simu yake kabla ya kupiga au kupokea simu.

Mfumo wa data wa TrueCaller ni mfumo ambao  watumiaji wake wanasaidiana kupeana taarifa za data za watu walio kwenye simu zao.

Unapopakua programu hiyo kutoka kwenye Playstore/App Store kisha ukaingia ndani kwa kuweka email na password yako, basi utakuwa umeruhusu wahusika kuona namba za watu ulionao kwenye kifaa husika na kuhifadhi taarifa hizo  kwenye kompyuta zao za kutunza kumbukumbu (servers).

▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬   

Pamoja na uzuri wa TrueCaller, yaweza kuwa imefika mahali sasa unawaza usalama wa namba yako ya simu au data zako na taarifa zako binafsi  na hivyo unatamani kujitoa au kufuta kabisa namba yako kwenye Mfumo wa TrueCaller
Leo tutakuelekeza namna ya kujitoa maana yawezekana hata kama   bado haujajiunga na app hiyo ila namba yako tayari imeunganishwa kwenye mfumo wa TrueCaller kupitia mtu mwingine mwenye number yako ya simu.

Kuna njia mbili za  kuiondoa namba yako kwenye mfumo wa TrueCaller, hii inategemea kama tayari ulijiandikisha kwenye huduma hii au haujajiandikisha lakini kumbuka kama kuna  mtu anayetumia app hii ya TrueCaller  na  ana namba yako basi  taarifa zako zimeingizwa pia kama alitoa 'access/Kibali' ya contacts list

Jinsi ya kujitoa au kutoa namba yako kutoka kwenye app ya TrueCaller

Kwa wale wenye akaunti za TrueCaller
1.Fungua app ya TrueCaller, nenda kwenye alama ya nukta tatu upande wa kushoto juu.
2.Kisha nenda Settings, kisha About, na hapo utaona chaguo la ‘Deactivate Account’ yaani futa akaunti…
3.Ata ukishafuta akaunti yako, yaani ‘deactivate account’ bado namba yako inaweza kuwa kwenye data za TrueCaller. Na hapa ndio inabidi uchukue hatua inayofanana na wale ambao hawana akaunti ya TrueCaller.
▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬   

Kwa wale wasio na akaunti ya TrueCaller au wamefuta/deactivate akaunti zao

1.Hatua inayofuata ni kuondoa namba kwenye mfumo wa kompyuta (servers) za huduma ya TrueCaller.
2.Nenda kwenye tovuti ya TrueCaller huduma ya kuondoa namba (Unlist)
3,Ukifika hapa andika namba yako ya simu, chukua hatua za kuonesha ya kwamba wewe ni binadamu (captcha) na kisha bofya ‘Unlist’
Share To:

msumbanews

Post A Comment: