Na Ferdinand Shayo,Killimanjaro.

Mkuu wa Wilaya ya Mwanga  Thomas Apson  ameteketeza  kwa moto nyavu aina ya makokoro na vyandarua vya kujikinga na mbu vinavyotumika kwa uvuvi haramu vilivyokamatwa katika oparesheni  inayoendelea  katika vijiji vinavyolizunguka bwawa hilo vyenye thamani vya shs.39.3mil.

Apson  amesema kuwa  katika oparesheni hiyo  wavuvi haramu 14 katika bwawa hilo wametiwa mbaroni kwa kuwatishia polisi wenye silaha waliokuwa doria na kuwataka waweke silaha ili  wazichape ngumi kavu kavu.

Afisa Tarafa ya Lembeni Bw Gikila Salisali  amesema, baadhi ya watumishi wa umma  wasiokuwa waaminifu wamekuwa kikwazo katika vita hivyo kwa  wanashirikiana na wavuvi haramu na kuiomba serikali iwape boti ili kuimarisha doria ndani ya  bwawa.

wananchi wa vijiji hivyo bi eda eliakimu na bakari kingazi wakazi wa nyumba ya Mungu wameipongeza serikali kwa kutangaza upya vita hivyo ambavyo wamesema vinaweza kusaidia kupunguza kasi ya uvuvi haramu ambao umekuwa tishio kwa samaki wachanga ambao  wangeweza  kubadili maisha yao.
Share To:

msumbanews

Post A Comment: