Rais Magufuli amemteua Charles Kichere kuwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kuanzia leo  akichukua nafasi iliyoachwa wazi na Profesa Mussa Assad ambaye muda wakeu unaisha kesho.


Viongozi wengine walioteuliwa ni Majaji 12 wa Mahakama Kuu, Balozi wa Tanzania nchini Kuwait ( Mhandisi Aisha Amuru ), Kamishna wa Kazi (Kanari Francis Leonard Mbindi ) na Katibu Tawala mkoa wa Njombe (Katalina Tengia Levekati ). 

Viongozi wote walioteuliwa leo na mheshimiwa Rais Magufuli wataapisha kesho asubuhi saa tatu na nusu viwanja vya Ikulu.

Share To:

msumbanews

Post A Comment: