WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa, Ieo Oktoba 29, 2019 amerejea nchini akitoka Baku nchini, Azerbijan ambako alimwakilisha Rais Dkt. John Pombe Magufuli katika mkutano wa 18 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Nchi zisizofungamana na upande wowote.

Baada ya kuwasili katika uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Waziri Mkuu amepokelewa na Naibu Spika wa Bunge Dkt. Tulia Ackson Mwansasu pamoja na viongozi wengine wa Mkoa wa Dar es salaam.

Awali, Mheshimiwa Majaliwa alimwakilisha Rais Dkt. John Pombe Magufuli katika Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Mataifa ya Afrika na Urusi uliofanyika katika mji wa Sochi nchini Urusi.

 (mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU
Share To:

msumbanews

Post A Comment: