Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan leo Sept 03,2019 amemuwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe magufuli kwenye Shuhuli ya kuaga Mwili wa Mwanasiasa Mkongwe Nchini Marehemu Ibrahim kaduma.

Katika salam zake za pole kwa Wanafamilia, wafiwa na Watanzania wote kwa Ujumla, Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan amewaomba kuwa na Subira na Uvumilivu katika kipindi hiki cha Maombolezo na kumuomba Mwenyezi Mungu kuwapa nguvu na Moyo wa Subira.

Wakati wa Uhai wake Marehemu Ibrahim Kaduma aliwahi kuwa Mwanasiasa pamoja na kupitia ngazi mbali mbali za Uongozi hapa nchini.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akitoa Heshima za Mwisho mbele ya Jeneza lenye Mwili wa Mwanasiasa Mkongwe Nchini Marehemu Ibrahim Kaduma katika Kanisa la KKKT Makongo Juu leo Sept 03,2019 ambapo Makamu wa Rais amemuwakilisha Rais Dkt. John Pombe Magufuli kwenye Msiba huo.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akisani kitabu cha kumbukumbu ya maombolezo kufuatia kifo cha Mwanasiasa Mkongwe nchini Marehemu Ibrahim Kaduma alipowasili katika Kanisa la KKKT Makongo Juu kwa ajili ya kumuwakilisha Rais Dkt. John Pombe Magufuli kwenye Shuhuli ya kuaga Mwili wa Mwanasiasa huyo leo Sept 03,2019. Kushoto ni Dkt. Alex Malasusa Askofu wa KKKT Dayosis ya Mashariki na Pwani.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimfariji, Mjane wa Marehemu Marehemu IBrahim Kaduma katika Kanisa la KKKT Makongo Juu, jijini Dar es salaam leo Sept 03,2019.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Dkt. Alex Malasusa Askofu wa KKKT Dayosis ya Mashariki na Pwani alipowasili katika Kanisa la KKKT Makongo Juu kwa ajili ya kumuwakilisha Rais Dkt. John Pombe Magufuli kwenye Shuhuli ya kuaga Mwili wa Mwanasiasa Mkongwe Marehemu IBrahim Kaduma leo Sept 03,2019.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na kuwapa pole Baadhi ya Wajukuu na Vitukuu vya Mwanasiasa Mkongwe Nchini Marehemu IBrahim Kaduma wakati wa shuhuli ya kuaga Mwili wa Mwanasiasa huyo leo Sept 03,2019 katika kanisa la KKKT Makongo Juu, Makamu wa Rais amemuwakilisha Rais Dkt. John Pombe Magufuli kwenye Msiba huo
Share To:

TANGA RAHA BLOG

Post A Comment: