Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa
akizungumza na Cherie Blair ambaye ni Mke wa Waziri Mkuu wa Zamani wa
Uingereza, Tony Blair walipokutana katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa
Kigali nchini Rwanda April 8, 2019. Majaliwa na Cherie walikuwa wakitoka
kuhudhuria hafla ya kumbukumbu ya miaka 25 ya mauaji ya kimbari nchini humo
iliyofanyika April 7, 2019. Katikati ni Balozi wa Tanzania nchini Rwanda,
Ernest Mangu. Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu
| Waziri
 Mkuu akiwa katika picha ya pamoja na Timu ya Serengeti Boys .katika 
Ofisi ya Ubalozi wa Tanzania. Kigali Rwanda April 7/2019 
PICHA NA OFISI YA WAZIRI MKUU 
 | 
*Asema Watanzania wanamatumaini makubwa kwao, waongeze bidii,
WAZIRI
 MKUU, Kassim Majaliwa ametembelea kambi ya timu ya Taifa ya vijana 
wenye umri wa chini ya miaka 17 na kuwaeleza kuwa Watanzania 
wanamatumaini makubwa dhidi yao, hivyo waongeze bidii.
Alitembelea
 kambi hiyo Serengeti Boys iliyoko katika jiji la Kigali nchini Rwanda. 
Waziri Mkuu alikwenda Rwanda Aprili 7, 2019 kumuwakilisha Rais Dkt. John
 Magufuli kwenye kumbukumbu za miaka 25 ya mauaji ya Kimbari.
Akizungumza
 na wachezaji hao jana (Jumapili, Aprili 8, 2019) Waziri Mkuu aliwataka 
vijana wanaounda timu hiyo ya Serengeti Boys wahakikishe wanafanya 
mazoezi ya kutosha ili waweze kushinda mechi zinazofuata.
“Watanzania
 wanamatumaini makubwa dhidi yenu nasi tunazidi kuwaombea kwa Mwenyezi 
Mungu muweze kuibuka na ushindi katika michezo yenu iliyobakia 
itakayowawezesha kushiriki mashindano ya kombe la dunia.”
Kadhalika,
 Waziri Mkuu alitumia fursa hiyo kuipongeza timu hiyo ya Serengeti Boys 
kwa namna wanavyoitangaza nchi kimataifa kupitia kwenye mashindano 
mbalimbali wanayoshiriki na kuibuka na ushindi.
Waziri
 Mkuu alisema endapo timu hiyo ya Taifa ya vijana ya Serengeti Boys 
itaibuka na ushindi katika michezo yake miwili itakuwa imekata tiketi ya
 kushiriki mashindano ya dunia huko nchini Brazil kwa vijana wa umri wa 
miaka 17.
Kwa upande wao,
 wachezaji na uongozi wa timu ya Serengeti Boys walimkabidhi Waziri Mkuu
 kombe walilolipata baada ya kuichapa timu ya Rwanda katika mashindano 
maalumu kwa ajili ya kujiandaa na AFCON-U17.
Mashindano
 hayo maalumu ya Kimataifa yalishirikisha timu za umri wa chini ya miaka
 17 kutoka nchi tatu ambazo ni Tanzania, Cameroon na wenyeji Rwanda, 
ambapo Serengeti Boys ilishinda mabao mawili kwa moja dhidi ya Cameroon 
na kutoka sare ya mabao matatu kwa matatu na Rwanda.
Pia,
 wachezaji hao wamemuahidi Waziri Mkuu kwamba watajitahidi kadiri ya 
uwezo wao kuhakikisha wanaibuka na ushidi katika mechi zilizobakia ili 
waweze kushiriki kombe la dunia. “Hatutawaangusha Watanzania.”
Awali,
 Waziri Mkuu alimshukuru Balozi wa Tanzania nchini Rwanda, Mheshimiwa 
Balozi Ernest Mangu pamoja na maofisa wa ubalozi na Watanzania waishio 
Rwanda kwa kuendelea kuipa moyo Serengeti Boys.  
 (mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
JUMATATU, APRILI 9, 2019.
Post A Comment: