Mchekeshaji au mtu maarufu kwa sasa mtandaoni, Pierre Liquid anazidi kugonga vichwa vya habari, na hii ni baada ya kuwasilini Bungeni Jijini Dodoma.


Pierre ambaye amekuwa akiwavutia wengi kutokana na vituko vyake ameonekana katika video ya pamoja na Spika wa Bunge, Job Ndugai na Naibu wake, Dkt. Tulia Ackson.

Utakumbuka wiki iliyopitia Ikulu Dar es Salaam, Makamu wa Rais Mama Samia alieleza kutambua mchango wa Pierre kwa kuhamasisha watu kwenda kutazama mchezo kati ya Uganda na Taifa Stars ambayo ilifanikiwa kufuzu AFCON baada ya miaka 39.
Share To:

msumbanews

Post A Comment: