Na Ferdinand Shayo, Arusha.

Chama cha Mapinduzi Wilaya ya karatu  kimeonya baadhi ya watendaji wanaohujumu miradi ya maendeleo ikiwemo miradi ya maji, barabara ambayo inalenga kutatua changamoto za wananchi.

Mwenyekiti wa Ccm Wilayani hapo Lucian  Akonaay amesema kuwa wanaohujumu miradi watachukuliwa hatua kwani wananchi bado wana imani na chama hicho katika kuhakikisha kuwa wananchi wanapata huduma muhimu za kijamii ikiwemo maji na miundombinu ya barabara pamoja na huduma za afya.

Akonaay Amesema kuwa chama hicho kimeandaa utaratibu wa kutembelea miradi ya maendeleo  na kujihakikishia kuwa iwapo inatekelezwa kwa viwango stahiki na kwa wakati uliopangwa

Katibu wa CCM Karatu  Solomon Itunda amesema Kuwa viongozi wa chama wamekua wakikagua maendeleo ya miradi pamoja na kuhakikisha kuwa wananchi wanapata huduma bora ikiwa ni pamoja na kutoa mapendekezo kwa viongozi wa serikali.

Diwani Mteule wa kata ya Baray kupitia  Chama hicho Elitumaini Rweyemamu amesema kuwa wamejiandaa kusimamia utekelezaji na kutatu kero za wananchi ili kuboresha huduma za kijamii.

Kwa Upande wake Mkazi wa Karatu ameipongeza serikali kwa kuhakikisha upatikanaji wa maji kwa kuchimba visima na kuiomba iongeze visima na mabomba hususan kwenye maeneo yenye watu wengi
Share To:

msumbanews

Post A Comment: