Leo Jumamosi 21/07/2018 tunatarajia kuanza Mchakato wa Kutafuta vipaji vya Michezo katika Wilaya ya Hai , Mkoani Kilimanjarokwa kuzindua Michuano ya Mpira wa Miguu kwa Kata ya Masama Rundugai itakayoshirikisha Timu nane na moja Timu moja mwalikwa kutoka Wilaya ya jirani ya Simanjiro.

Tunaanza na kata ya Masama Rundugai kama kata ya kufanyia UTAFITI tafiti wa tutakachokwenda kufanya kwa kata zote 17 za jimbo la HAI kwa ajili ya Kujipanga kuanza Michuano ya Mpira wa Miguu Kwa Wilaya ya Hai kabla ya Kumaliza mwaka 2018.

Nawashukuru Wadau wa Michezo Wilaya ya Hai, Marafiki zangu kwa kunipa support ya Baadhi ya Vifaa, na nawashukuru wana Hai kwa kukubali Kuungana Nami katika Safari ya kuwafikia vijana wengi wenye vipaji vya Michezo na sanaa.

Nawatakia Mapumziko Mema ya Wiki, na kribuni tujenge Msingi wa Hatma ya Maendeleo ya Vijana wetu Wilaya ya Hai, Mkoani Kilimanjaro.

 Jerry Muro

Share To:

msumbanews

Post A Comment: