Klabu ya Singida United imefanikiwa kumsajili, Feisal Salum Abdalah maarufu kama ‘Fei Toto’ kutokea JKU kwa kandarasi ya miaka mitatu.

Meneja wa Singida United, Hemedi Selemani Morocco amefanikiwa kumpata kijana huyo kwa kushirikiana na JKU na kuridhia gharama zilizo hitajika.

Kiungo huyo mahiri wa JKU na timu ya taifa ya Zanzibar, Zanzibar Heroes pamoja na Taifa Stars, Fesal Salum “Fei Toto” alifanikiwa kutwaa tuzo ya mchezaji bora kupitia michuano ya Mapinduzi Cup.
Share To:

msumbanews

Post A Comment: