Mgeni
Rasmi Mkuu wa Wilaya ya Arusha Mhe. Fabian Daqqaro (katikati) akizindua
usajili na utoaji wa vitambulisho kwa wafanyabiashara wadogo walio
kwenye sekta isiyo rasmi wakati wa hafla fupi ya uzinduzi huo
iliyoandaliwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA). Wa pili kushoto ni
Meneja wa TRA Mkoa wa Arusha Bw. Faustine Mdessa.
Kiongozi
wa Kikundi cha Levolosi Machinga Group Bw. Hassan Shayo maarufu kama G
akikabidhiwa kitambulisho wakati wa hafla fupi ya uzinduzi wa usajili na
utoaji wa vitabulisho kwa wafanyabiashara wadogo walio kwenye sekta
isiyo rasmi iliyoandaliwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA). Hafla
hiyo imefanyika leo jijini Arusha na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali
na wafanyabiashara wadogo.
==>> Unaweza Kuidownload << kwa Kubofya Hapa>>
==>> Unaweza Kuidownload << kwa Kubofya Hapa>>
Mgeni
Rasmi Mkuu wa Wilaya ya Arusha Mhe. Fabian Daqqaro (wa tatu kulia) akiwa
ameketi meza kuu wakati wa hafla fupi ya uzinduzi wa usajili na utoaji
wa vitambulisho kwa wafanyabiashara wadogo walio kwenye sekta isiyo
rasmi iliyoandaliwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA). Hafla hiyo
imefanyika leo jijini Arusha na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali na
wafanyabiashara wadogo.
Baadhi
ya wafanyabiashara wadogo walio kwenye sekta isiyo rasmi wakifuatilia
kwa makini hotuba ya mgeni rasmi (hayupo pichani) wakati wa hafla fupi
ya uzinduzi wa usajili na utoaji wa vitambulisho kwa wafanyabiashara hao
iliyoandaliwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA). Hafla hiyo
imefanyika leo jijini Arusha na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali na
wafanyabiashara wadogo.
Mgeni
Rasmi Mkuu wa Wilaya ya Arusha Mhe. Fabian Daqqaro (katikati) akiwa
katika picha ya pamoja na baadhi viongozi mbalimbali na wafanyabiashara
wadogo walio kwenye sekta isiyo rasmi baada ya uzinduzi wa usajili na
utoaji wa vitambulisho kwa wafanyabiashara hao ulioandaliwa na Mamlaka
ya Mapato Tanzania (TRA). Hafla hiyo ya uzinduzi imefanyika leo jijini
Arusha na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali na wafanyabiashara wadogo
Na Veronica Kazimoto,Arusha,
Wito
umetolewa kwa wafanyabiashara wadogo walio kwenye sekta isiyo rasmi
hususani wamachinga kujisajili na hatimaye kupatiwa vitambulisho maalum
kwa lengo la kusaidia biashara zao kutambulika, kukopesheka na
kurahisisha mawasiliano ya usimamizi wa biashara hizo.
Akizungumza
wakati wa uzinduzi wa usajili na utoaji wa vitambulisho kwa
wafanyabiashara wadogo uliofanyika leo mkoani Arusha, Mwakilishi wa Mkuu
wa Mkoa huo Mhe. Fabian Daqqaro amesema ni muhimu wafanyabiashara
kutumia fursa hii ya kujisajili ili kurasimisha biashara zao.
“Ni
matumaini yangu kuwa, wafanyabiashara wengi wadogo wadogo mkoani hapa,
mtatumia fursa hii kujisajili kwa sababu ninafahamu wengi wenu malengo
yenu siyo kuwa wafanyabiashara wadogo muda wote, bali mtakuza biashara
zenu na kuwa wafanyabiashara wakubwa na hii itawezesha kuchangia mapato
ya Serikali,” alisema Daqqaro.
Kwa
upande wake Kamishna Msaidizi wa Kodi za Ndani kutoka Mamlaka ya Mapato
Tanzania (TRA) Abdul Zuberi ameeleza kuwa, zoezi hili la kuwasajili na
kuwapatia vitambulisho wafanyabiashara wadogo limetokana na juhudi za
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Joseph
Magufuli.
“Ni
ukweli usiopingika kwamba, Rais wetu kwa nyakati tofauti amekuwa
akiwapigania na kutaka wafanyabiashara wadogo wadogo kutambulika rasmi
na kupatiwa vitambulisho ikiwa ni pamoja na kutafutiwa maeneo rafiki ya
kufanyia biashara zao,” alisema Zuberi.
Ameongeza
kuwa, kutokana na juhudi hizo za Rais Magufuli, Serikali kupitia Kikao
cha Bunge la Bajeti la Mwaka wa Fedha 2017/2018, ilifanya marekebisho
mbalimbali ya Sheria ya Usimamizi wa Kodi ya Mwaka 2015 ambapo moja ya
marekebisho hayo ni kuwatambua na kuwapatia vitambulisho maalum
wafanyabiashara wadogo walio kwenye sekta isiyo rasmi na jukumu hili
limekasimiwa kwa Mamlaka ya Mapato Tanzania.
Zuberi
alisema kuwa, zoezi hili limeshafanyika katika Mkoa wa Dar es Salaam na
Mwanza na sasa limefanyika mkoani Arusha ambapo jumla ya vikundi 125
vya wafanyabiashara wadogo vinatarajiwa kusajiliwa na hadi sasa vikundi
25 vimeshatambuliwa vikiwa na jumla ya wafanyabiashara wadogo takribani
3,600 na kwa uwakilishi wafanyabiashara 100 wamepatiwa vitambulisho
jijini hapa.
Naye
Kiongozi wa Wamachinga mkoani Arusha Fredson Athumani, ameishukuru
Serikali kwa kuwatambua rasmi na kusisitiza kuwa, atahakikisha
anashirikiana na viongozi wenzake pamoja na Serikali kuwahamasisha
wafanyabiashara wote wadogo kusajiliwa na kupata vitambulisho maalumu.
Zoezi
la usajili na utoaji wa vitambulisho kwa wafanyabiashara wadogo walio
kwenye sekta isiyo rasmi linafanyika chini ya Mamlaka ya Mapato Tanzania
kwa kushirikiana na Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA), Serikali
za Mitaa, Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA) pamoja na Idara
ya Uhamiaji.
Post A Comment: