Malkia wa filamu, Jacqueline Wolper ameamua kunyamaza na kusitisha malumbano yaliyoanza kwenye mitandao kati yake na aliyekuwa mpenzi wake wa zamani, Harmonize.

Malumbano hao yasiokuwa ya kawaida yameanza Jumanne hii baada ya Harmonize kupost list ya wanaume aliodai wamewahi kutembea na mpenzi wake huyo wazamani, Jacqueline Wolper.

Hatua hiyo ilimfanya Wolper kuibuka na kuanza kuandika mambo mbalimbali mabaya akimtuhumu muimbaji huyo wa wimbo, DM Chick, huku akidai ndiye aliyesababisha alumbane na Sarah.

Alhamisi hii Wolper aameamua kuwa mpole kwa kufunga malumbano hayo baada ya Harmonize kudai ataandaa list C ya wanaume aliotembea na mrembo huyo kutoka katika kiwanda cha filamu.

“Mungu nifundishe kunyamaza, we ndio unaujua ukweli 🙏#Najifunzakuheshimkilangaziiliyonifikishanilipo  #NdiomaanataupambanesiwezkushukaatanishushaMungupekee #jifunzekuheshimkilangaziiliyokufishaulipokamweutoteterekakwajarbulolote  #MunguwanguwaushindiwewenijbuToshaNimekukabidhiwewekilaktu🙌🙏,”

Baadhi ya mashabiki katika mitandao ya kijamii wanadai Harmonize anamchokoza Wolper ili apate kiki za project yake mpya.

Muimbaji huyo siku ya leo ameachia kolabo yake ya wimbo ‘Pull Up’ akiwa ameshirikiana na Eddy Kenzo
Share To:

msumbanews

Post A Comment: