Bunge limebadilisha ratiba ili kuruhusu waumini wa dini ya Kiislamu kushiriki kikamilifu mfungo mtukufu wa Ramadhan bila kuathiri shughuli za chombo hicho cha Dola.

Utenguaji wa kanuni hizo umefanywa bungeni leo Jumatano Mei 16, 2018 na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Jenista Mhagama na kuungwa mkono na wabunge.

Kwa mujibu wa Mhagama, ratiba iliyobadilika ni ya kipindi cha mchana ambapo sasa Bunge litaanza saa 10:00 jioni badala ya saa 11.00 jioni na kumalizika saa 12.00 jioni badala ya saa 1.45 usiku.

Amesema mara baada ya kumalizika kwa mfungo huo, ratiba itarudi kama kawaida.
Share To:

msumbanews

Post A Comment: