Wema
 Sepetu amempiga dongo Mange Kimambi kufuatia maandamano aliyokuwa 
akiyahamasisha kupitia mitandao ya kijamii akiwataka Watanzania 
waandamane kutokufanikiwa.
Mange
 alikuwa akiwashawishi Watanzania kuandamana leo katika maadhimisho wa 
miaka 54 ya Muungano wa Tanzania ikiwa ni ishara ya kupinga baadhi ya 
mambo yanayofanywa na serikali ya awamu ya tano, lakini hata hivyo, 
maandamano hayo hayajafanyika katika kiwango kilichokuwa kikidhaniwa.
Watu
 wengi leo walikaa majumbani mwao wakihofia kutoka nje kutokana na 
polisi kutishia kuwashughulikia wale wote watakaoandamana, hali 
iliyopelekea baadhi ya watu kukatisha shughuli zao.
Kupitia
 ukurasa wake wa Instagram Wema amesema kuwa alisitisha safari yake ya 
kwenda Arusha kutokana na hofu kuwa kungekuwa na maandaamano, kumbe 
hakuna kitu chochote.
“Watu
 Tukajua Kuna Maandamano mpaka Safari tukazihairisha… Kumbe hamna kitu… 
Ila utani tuweke pembeni wengi wetu tulishtushwa… But one thing y’all 
have to understand is Wa Moja Wa Moja tu… Aliepewa kapewa… And Kamwe 
huwezi shindana na POWER.”
Aliendelea
 kusema, “ARUSHA… Tunaomba Radhi… We had to Cancel our Trip sababu ya 
Haya Mambo ya Uongo na Kweli… But Tunakuja Soon tutawajulisha wapendwa 
wetu.”
Licha
 ya kuwa Wema hakumtaja Mange katika ‘post’ yake, lakini ni dhahiri kuwa
 dongo hili limeelekezwa kwa Mange kwani ndiye alikuwa mhamasishaji mkuu
 wa maandamano haya ambayo Wema amesema ni ya uongo.
A

Post A Comment: