Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP) Simon Sirro amesema Jeshi lake liko imara kweli kweli katika kupambana na watu wanaotaka kuleta uvunjifu wa amani nchini, huku akiwasii wanaotaka kuandamana kuacha mara moja kwani kitakachowapata wasije kulaumiana

IGP Sirro ametoa kauli hiyo leo (Aprili 7, 2018) wakati akitoa salamu zake kwa Rais Dkt. Magufuli katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid uliopo mjini Arusha baada ya uzinduzi wa nyumba za askari na kushuhudia maonesho ya utayari ya jeshi hilo katika kukabiliana na uhalifu.

"Mhe. Rais Magufuli Jeshi lako la  Polisi liko imara tena imara kweli kweli, kwa kupambana na watu wote wanaotaka kuleta uvunjifu wa amani hapa nchini na kwa bahati nzuri wananchi wapo pamoja na wewe Rais na Jeshi lako.
" Ila naomba nitoe ushauri wa bure kwa wale wote wenye nia ya kuchafua amani ya nchi yetu , ni wasii waache mara moja na kama wataona ushauri huo hauna maana basi baadae tusilaumiane", amesema IGP Sirro.

Pamoja na hayo, IGP Sirro ameendelea kwa kusema "upo uhamasishaji kwenye mitandao, na hili niseme  naamini wameshaandamana kwenye mitandao na wameshamaliza maandamano yao. Kwa hiyo la msingi sana tujenge nchi yetu".

Kwa upande mwingine, IGP Sirro amesema katika kipindi cha mwezi Januari hadi Februari mwaka 2018 kuna jumla ya matukio ya jinai yaliyoripotiwa ni 96,363 ikilinganishwa na matukio 104,073 yaliyoripotiwa kipindi kama hicho mwaka 2017.
Share To:

msumbanews

Post A Comment: