Inawezekana unatumia kikombe cha chai  au kikombe cha  kahawa kila siku asubuhi, wengi wao hutumia maji ya kawaida ili kuanza siku vizuri. Hivi vitu vimekuwa ndio tabia ya kila siku , hata hivyo wachunguzi wanasema kunywa maji ya uvuguvugu  asubuhi wakati tumbo halina kitu unapata faida  za kiafya zaidi.

Madactari wanashauri kutumia maji ya uvuguvugu   yaliotiwa  liau au ndimu ili  kupunguza radical ndani ya mwili. Kutumia maji ya moto  inaongeza na kufungua utumbo ili kukufanya wewe upate haja kubwa kwa urahisi

Na hapa kuna faida 7  za vitu vinavyotokea katika mwili wako utakapoanza kutumia maji ya moto kila asubuhi.

1. Yanasaidia kuondoa Mikunjo.
Kunywa maji inakusaidia usizeeke mapema,hakuna mtu anaependa kuzeeka mapema.hata hivyo  sumu ndani ya mwili inaweza kukufanya uzeeke mapema. Wakati mwili wako unapotoa sumu  utapunguza magonjwa   na uzee. Maji ya  moto usaidia kuondoa sumu na yanasafisha kabisa. Zaidi sana  yanasaidia kurejesha cells za ngozi iwe inaonekana kuvutia na nyororo.

2. Huepusha maumivu.
Dawa ya nguvu  ya kutegemea kupunguza maumivu wakati wa hedhi ni maji ya moto, yanafanya misuli ya tumbo  irelax  na kupungua kwa maumivu. Maji ya moto husaidia mzunguko kapirali  na misuli katika mwili pia.

3. Yanasaidia kupunguza uzito.
Inawezekana unajaribu kupunguza uzito  na umesikia kuwa maji ya moto asubuhi yanaweza kuwa ni msaada mkubwa kwako. Hii ni kweli., maji ya moto yanaongeza joto la mwili, ambalo  linabadilisha ongezeko la  kiasi cha metabolic, kuongezeka kwa metabolic  mwili unakuwa na uwezo wa kuchoma carories siku nzima.

Kama ukianza na kunywa maji ya moto yenye limau. Utausaidia mwili wako kuvunja vunja mafuta  yalioko ndani.

4. Yanaboresha digestion.
Unapokunywa maji ya moto asubuhi unastimulate  digestion yako  na  kuusaidia mwili kuwa na digestion bora. Kunywa maji ya baridi ya ya kula chakula inaweza kusimamisha digestion yako, na mwili wako ukawa  na matatizo, maana maji yabaridi yana gandisha mafuta yalioko kwenye chakula na kufanya digestion iwe ngumu kwako. Ni bora ukatumia maji ya moto kuliko ya baridi.

5. Yanaboresha mzunguko wa damu mwilini.
Kunakuwa na mlimbikizo wa  mlolongo wa nervous na mlimbikizo wa mafuta mwilini , lakini unapotumia maji ya moto yanaenda kuondoa hio migandanizo. Hii process inaflash sumu yote  ndani ya mwili na kuufanya mzunguko wa damu kuwa mzuri na kufanya misuli kupumzika.

6. Yanakufanya Upate Usingizi Vizuri.
Unapotumia maji ya moto  wakati wa chakula cha usiku, na kabla ya kwenda kulala, utaufanya mwili wako kurelax na  kulainisha nerves zako. Hii itakufanya ulale vizuri na kuwa na utashi mzuri kwa ajili ya kuamka asubuhi.

Tumeona  faida 7 za kushangaza   ambazo zinaweza kutokea katika mwili wako utakapoanza kutumia maji ya moto kila asubuhi na jioni . Anza sasa kutumia maji ya moto kila siku ili uone faida  nzuri  tulizosoma hapo juu kwa ajili ya manufaa yako .

Mimi nimeanza  kujaribi na nimeona kuna faida, anza na wewe leo.
Share To:

msumbanews

Post A Comment: