Na HERI SHAABAN

TAASISI ya Fahari Tuamke Maendeleo watoa misaada mbalimbali ya vyakula na vifaa vya Shule kwa Wanafunzi wa shule ya Msingi Bangulo Gongolamboto Wilaya ya Ilala.


Misaada hiyo ulitolewa shuleni hapo  katika siku Maalum ya matendo mema Duniani ambapo Taasisi ya Fahari Tuamke Maendeleo kila mwaka imetenga siku hiyo kutoa misaada kwa makundi maalum pamoja na Wanafunzi wenye Mazingira magumu.


Akizungumza shuleni hapo mara baada kutoa msaada huo Mkurugenzi wa Fahari Tuamke Maendeleo Neema Mchau, alisema  madhimisho ya siku ya matendo mema Duniani kwa Wilaya ya Ilala yatadhimishwa wiki hii  ukumbi wa John Bosco Upanga kabla kufika siku hiyo wanatoa chochote walichojaliwa kwa Jamii.


"Fahari Tuamke Maendeleo Leo tumetoa msaada shule ya Msingi Bangulo Gongolamboto misaada tuliotoa Leo kwa wanafunzi wenye Mazingira magumu  Vifaa vya shule daftari ,Viatu kila mwanafunzi pamoja   na  unga wa sembe " alisema Neema


 Neema mchau alisema Taasisi ya Fahari Tuamke Maendeleo ni Taasisi ya kijamii inashirikiana na Serikali katika Shughuli mbalimbali  ikiwemo kuwekeza sekta ya Elimu Wilaya ya Ilala.


Alisema Fahari Tuamke Maendeleo tumejenga tabia kila mwaka tunasaidia jamii aidha sekta ya elimu na makundi maalum.


Alisema shule Msingi Ulongoni Gongolamboto ina wanafunzi waliopo katika Mazingira magumu kutokana na Wazazi wao kukosa uwezo wa Vifaa vya shule ikiwemo daftari,sare za shule ,viatu  Fahari Tuamke Maendeleo imekuwa mlezi wa Wanafunzi hao katika juhudi za kuisaidia Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa TANZANIA kuwapatia vifaa vya Shule Ili washike elimu ije kuwakomboa




Share To:

JUSLINE

Post A Comment: