Rais
Samia Suluhu Hassan katikati akikata utepe Ishara ya uzinduzi wa
hospitali ya wilaya Njiro Jijini Arusha,kushoto kwake ni waziri wa
Tamisemi Ummy Mwalimu,Mkuu wa mkoa wa Arusha John Mongela na mbunge wa
Arusha Mrisho Gambo
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Samia Suluhu Hassan akisalimiana na mmoja wa akina mama kati
waliojifungua katika hospital ya wilaya aliyoizindua leo up 17/10/2021
Jijini Arusha iliyojengwa kwa tsh bil.2.5
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Samia Suluhu Hassan akisalimiana na mmoja wa akina mama kati
waliojifungua katika hospital ya wilaya aliyoizindua leo 17/10/2021
Jijini Arusha iliyojengwa kwa tsh bil.2.5
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan
akimkabidhi hundi kwa vikundi vya wanawake,vijana na walemavu wa kata ya
Themi Njiro Jijini Arusha ya shilingi mil.387,380,615 (NMB)mara baada
ya kuzindua hospital ya wilaya leo 17/10/2021 Jijini Arusha
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu
Hassan akimkabidhi hundi kwa vikundi vya wanawake,vijana na walemavu wa
kata ya Themi Njiro Jijini Arusha ya
shilingi mil. 661,852,000( NBC)mara baada ya kuzindua hospitali ya
wilaya 17/10/2021 Jijini Arusha
Rais
wa Jamhuri ya Tanzania Samia Suluhu Hassan, amekagua Kituo na 5 Cha
kusukumia maji maeneo ya chekereni ikiwa ni sehemu ya mradi mkubwa wa
maji wa bil.520 ,katika eneo la ARUMERU na Jiji la Arusha,ambapo ni
mradi wa pili wa maji kwa ukubwa nchini Tanzania baada ya mradi wa maji
uliopo mkoa wa Tabora
Akizungumza
na wananchi kata ya Mlangarini wilaya ya Arumeru, Rais Samia alisema
kuwa changamoto kubwa ya jiji la Arusha ilikuwa maji na barabara ,ambapo
maji wameshautatua kupitia mradi utakaokamilika mwakani,na kusema
suala la barabara watakaa na Uongozi wa mkoa pamoja na Tanrod /Tarura
,kuangalia ni sehemu gani kuna changamoto
" Lengo la Serikali ni kuunganisha barabara za wilaya.alisema Samia.
Akitoa
taarifa ya Maendeleo ya mradi huo Mkurugenzi mtendaji wa
(AWSA)Justine Rujomba ,alisema kuwa Kituo hicho kina uwezo wa kupitisha
maji lita mil.80,000 ambapo wameweza kuchimba kutoka hai Umbali wa km
83, ambapo katika vijiji mradi huo utapitia navyo vitanufaika kwa kupata
maji
Rujoba alisema
kuwa chanzo kikubwa Cha maji ni visima virefu katika maeneo mbalimbali,
ambapo wamechimba visima 18 kutoka eneo la majimoto hai , ni km 83 hadi
mredi ulipo, na maji yake siyo ya chumvi ,hadi Sasa imekamilika kwa 75%
unategemewa kukamilika June mwakani 2022
Mradi wa Chekereni unavisima 41 na tenki la maji lenye ujazo wa lita milioni 3 pamoja na pampu za kusukuma maji.
Wakati
huohuo Rais Samia Suluhu Hassan alizindua hospital ya wilaya kata ya
njiro lililogarimu kiasi Cha Shi Bil.2.5, sambamba na kukabidhi hundi
za mikopo kwa wanawake,vijana na watu wenye ulemavu wenye jumla ya
sh.bil.1.3
Baadhi
ya wakazi watakaonufaika na mradi huo wameishukuru serikali ,kwani
karibuni wataanza kupata maji safi na salama, ambayo hayatakuwa na
athari za kiafya, kama kuharibu rangi ya meno yao.
Raia Samia anaendelea na ziara yake mkoani Arusha ambapo aliwasili jana jioni akitokea mkoa wa Kilimanjaro.
Post A Comment: