Naibu
Waziri Wa Maji Mhandisi Maryprisca Mahundi akizungumza na waandishi wa
habari baada ya kutembelea miradi ya maji inayotekelezwa na Mamlaka ya
Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) akisisitiza kwa
wakandarasi kukamilisha kwa wakati mradi wa usambazaji maji wa B2F
kutoka Chuo Kikuu hadi Bagamoyo Wenye thamani ya Bilion 65.
Naibu
Waziri Wa Maji Mhandisi Maryprisca Mahundi akipanda juu kukagua ujenzi
wa mradi wa maji inayotekelezwa na Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa
Mazingira Dar es Salaam (DAWASA). Maryprisca amesisitiza wakandarasi
kukamilisha kwa wakati mradi wa usambazaji maji wa B2F kutoka Chuo Kikuu
hadi Bagamoyo Wenye thamani ya Bilion 65.
Moja
ya tanki la ujazo wa Lita Milioni tano katika mradi wa usambazaji maji
wa B2F kutokea Chuo Kikuu hadi Bagamoyo linalojengwa katika eneo la
Tegeta A.
Naibu
Waziri wa Maji Mhandisi Maryprisca Mahundi amewataka wakandarasi wa
mradi wa uboreshaji maji kutola Chuo Kikuu cha Ardhi hadi Bagamoyo
kukamilika ndani ya wakati.
Mradi
huo wa uboreshaji maji kutoka Chuo Kikuu cha Ardhi hadi Bagamoyo
unatekelezwa na Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam
(DAWASA) kwa thamani ya Bilioni 65 ikiwa ni fedha za mkopp kutoka Benki
ya Dunia.
Akizungumza
wakati wa muendelezo wa ziara yake ya kutembelea miradi inayotekelezwa
na DAWASA, Naibu Waziri amesema mradi wa uboreshaji maji ni moja ya
miradi mikubwa inayotekelezwa kimkakati inayoenda kumtua mama ndoo
kichwani.
Mheshimiwa
Maryprisca amesema, Wizara bado inaendelea kuboresha huduma za maji kwa
wananchi na kukamilila kwa mradi huo kutasaidia kufanya maunganisho
mapya elfu sitini (60,000).
“Huu
mradi wa Kutokea Chuo Kikuu cha Ardhi hadi Bagamoyo utakapokamilika
utafanya maunganisho mapya elfu sitini (60,000) na hii haitakuwa mwisho
serikali tutaendelea kuboresha huduma kwa kuleta miradi mipya,”amesema
“Kukamilika
kwa mradi huu kutaenda kuondoa kero ya maji kwa wananchi hata wale wa
Goba ambao wamekuwa na changamoto ya maji kwa muda mrefu na ujenzi wa
matanki haya matatu utaenda kuondoa tatizo la maji sambamba na mgao,”
amesema
Mheshimiwa
Maryprisca amesisitiza kwa wakandarasi watakaoshindwa kukamilisha
miradi kwa wakati kuwa serikali haitawafumbia macho na itawachukulia
hatua ikiwemo kuvunja mikataba ili kulinda maslahi ya watanzania.
“Sisi
hatutaki wakandarasi wajanja wajanja katika kutekeleza miradi yetu na
hatutasita kuvunja mkataba tukiona mkandarasi anashindwa kutekeleza
makubaliano kwa wakati na hilo limeweza kutokea pia katika mradi wa
Same-Mwanga na Waziri Jumaa Aweso aliweza kuvunja mkataba nao,” amesema
Mheshimiwa Maryprisca.
Aidha,
amesema katika kutekeleza miradi mikubwa kama hii kunajitokeza
changamoto mbalimbali ikiwemo kuchelewa kwa msamaha wa kodi ila
amewahakikishia wakandarasi kuwa Wizara yake imeliona hilo na
limeshalifanyia kazi.
Mheshimiwa Maryprisca amewapongeza wananchi waliokubali maeneo yao kupita kwa mradi huo ambao utaondoa kero ya maji.
Naye
Mkurugenzi wa Miradi na Uwekezaji DAWASA, Mhandisi Ramadhani Mtindasi
amesema mradi huu umeanza ujenzi mwaka 2019 na unatarajia kukamilika
ndani ya miezi 24 ambapo mwishoni mwa mwaka huu mkandarasi anatakiwa
kukabidhi mradi huo.
Mtindasi
amesema watajenga matanki makubwa ya Lita Milioni 5 pia watajenga vituo
vya kusukumia maji (Booster station) na kulaza mabomba kwa umbali wa
Kilomita 1000.
“Tunatekeleza
mradi huu kwa fedha tulizofadhiliwa na Benki ya Dunia kiasi cha Bilioni
65 ambapo tutajenga matanki makubwa, vituo vya kusukumia maji (booster
station)na ulazaji wa mabomba na utaenda kutoa huduma kwa wateja elfu
sitini (60,000) kuanzia Chuo Kikuu cha Ardhi hadi Bagamoyo,” amesema
Mhandisi Mtindasi.
Mradi
huo utahusisha ujenzi wa matanki matatu yenye ujazo wa Lita Milioni 5,
vituo vya kusukumia maji vikubwa viwili (booster station) na italaza
mabomba kwa umbali wa Kilomita 1000 kuanzia Chuo Kikuu cha Ardhi hadi
Bagamoyo na utaweza kuunganisha wateja wapya 60,000.
Post A Comment: