Mshambuliaji
wa pembeni wa timu ya netiboli ya Uhamiaji ya Dar es salaam Fatuma
Chenge akijaribu kufunga mojawapo ya magoli ambapo Magereza walishinda
kwa magoli 37-36.
Mshambuliaji
wa pembeni wa timu ya netiboli ya Magereza Morogoro Naima Boli
akijaribu kufunga mojawapo ya magoli ambapo Magereza walishinda kwa
magoli 37-36
Afisa
Michezo wa Jiji la Arusha Benson Maneno akizungumza na waandishi wa
habari mara baada ya ufunguzi wa ligi ya netiboli katika uwanja wa
sheikh Amri Abeid jijini Arusha
Katibu
Mkuu wa CHANETA Judith Ilunda akizungumza na waandishi wa habari mara
baada ya ufunguzi wa ligi ya netiboli katika uwanja wa sheikh Amri Abeid
jijini Arusha
……………………………………………………………………
Na Mathew Kwembe, Arusha
Timu
zinazoshiriki mashindano ya ligi daraja la kwanza netiboli zimetakiwa
kuwatumia wachezaji wenye vipaji kutoka katika michezo ya UMISSETA ili
kuwawezesha wachezaji hao kukuza vipaji vyao lakini pia kuondokana na
mtindo wa kila mwaka kutegemea wachezaji hao hao.
Kauli hiyo
imetolewa jana jijini Arusha na Afisa Michezo wa Jiji hilo Benson Maneno
mara baada ya ufunguzi wa mashindano ya ligi ya netiboli uliofanyika
katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid.
Amesema kuwa wao kama jiji
la Arusha wameutumia mfumo huo ambapo wameweza kuchukua wachezaji wengi
waliowahi kushiriki michezo Michezo ya Umoja wa Shule za Sekondari
Tanzania (UMISSETA) ambayo ilimazika hivi karibuni mjini Mtwara.
Sambamba
na hilo, Maneno amewataka waandaaji wa ligi ya netiboli ambao ni
CHANETA kuhakikisha kuwa mashindano haya yasiwe yanafanyika mwezi wa
saba kwani taasisi nyingi za serikali zinashindwa kuleta timu.
“
Ni kipindi ambacho serikali inahamisha kutoka bajeti ya mwaka mmoja
kwenda mwaka mwingine, kwa mfano hapa tulitegemea Tanga Jiji wawepo, na
mashirika mbalimbali,” amesema Maneno na kuongeza:
“Wito wangu
kwa viongozi wa netiboli Tanzania wayatengeneze mashindano haya katika
kipindi ambacho serikali inatumia fedha zake.
Naye Katibu Mkuu
wa CHANETA Judith Ilunda amesema kuwa katika mashindano ya mwaka huu
walitegemea zishiriki timu 21 za wanawake na 5 za wanaume lakini sasa
hivi timu za wanawake zinazoshiriki ni 12 na nne za wavulana.
Amesema
michuano hii iliyoanza tarehe 19 julai itamalizika tarehe 30 juni
ambapo Bingwa atapatikana huku washindi wa nafasi za juu wataiwakilisha
nchi katika mashindano ya netiboli kwa nchi za Afrika mashariki, huku
timu sita za juu zitashiriki kwenye ligi ya netiboli ya muungano ambayo
imepangwa kufanyika mjini Zanzibar baadaye mwaka huu.
Katika
michezo mingine iliyochezwa jana, Timu ya Magereza ya Morogoro iliifunga
kwa tabu Uhamiaji ya Dar es salaam magoli 37-36, huku Mbeni JKT
ikiifunga Polisi Arusha magoli 66 Polisi Arusha 63.
Mashindano
haya yataendelea tena hapo kesho kwa michezo kadhaa ikiwemo mchezo kati
ya timu ngumu ya TAMISEMI QUEENS dhidi ya Polisi Arusha.
Post A Comment: