Mkuu wa Mkoa wa Tabora Dk. Balozi Batilda Buriani akimkabidhi Mwenge wa Uhuru 2021 Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dk.Binilith Mahenge katika Kijiji cha Mseko wilayani Iramba baada ya kuhitimisha mbio zake mkoani humo leo. Mwenge wa Uhuru ukiwa mkoani hapa unatarajiwa kupitia miradi mbalimbali yenye thamani ya Sh.8,182,219,653.99.
Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dk.Binilith Mahenge, akisoma taarifa ya mkoa wakati wa kupokea Mwenge wa Uhuru.
Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dk.Binilith Mahenge akimkabidhi Mwenge wa Uhuru 2021 Mkuu wa Wilaya ya Iramba Selemani Mwenda kwa ajili ya kuanza mbio zake wilayani humo
    Mwenge wa Uhuru ukipokelewa.
Mwenge wa Uhuru ukipokelewa.
Viongozi mbalimbali wakiwa katika mapokezi ya Mwenge wa Uhuru.
Viongozi mbalimbali wakipiga makofi kwenye mapokezi ya Mwenge wa Uhuru.
Utambulisho ukifanyika


Kamanda wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Singida, Kamishna Msaidizi Mwandamizi (SACAF) Ivo Ombella aliwa ameushika Mwenge wa Uhuru.


Askari wakiwa wameuzunguka Mwenge wa Uhuru kwa ajili ya usalama..



Mkuu wa Wilaya ya Iramba Selemani Mwenda, akizungumza baada ya kukabidhiwa Mwenge wa Uhuru.


Watumishi wa Idara  mbalimbali wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba wakiwa  kwenye mapokezi ya Mwenge wa Uhuru.
Wananchi na Vijana wa Skauti mapokezi wa Mwenge wa Uhuru.
Vijana wa Skauti wakimvika Skafu mmoja wa wakimbiza Mwenge wa Uhuru Kitaifa.
Vijana wa Skauti wakiimarisha ulinzi wakati wa kuupokea Mwenge baada ya kuwasili wilayani Iramba katika Kijiji cha Mseko.
Vijana wa Skauti  wakiwa imara wakati wa mapokezi wa Mwenge wa Uhuru.
 Mkuu wa Wilaya ya Iramba Selemani Mwenda , akikabidhiwa Mwenge wa Uhuru.
Mwenge wa Uhuru ukikabidhiwa kwa Watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba kabla ya kuanzwa kukimbizwa katika wilaya hiyo.


Ulinzi ukiimarishwa kwenye mapokezi hayo

 



Na Dotto Mwaibale, Iramba,  Singida.


SERIKALI Mkoa wa Singida kwa kushirikiana na wananchi mapema leo asubuhi wameupokea Mwenge wa Uhuru ukitokea mkoani Tabora.

Miradi  yenye  thamani ya Sh. 8,182,219,653.99 inatarajiwa kupitiwa na Mwenge wa Uhuru 2021, mkoani hapa ambao mbio zake zimeanza katika Wilaya ya Iramba.

Akizungumza baada ya kukabidhiwa Mwenge huo na Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Dk.Balozi Batilda Buriani katika Kijiji cha Mseko wilayani Iramba Mkuu wa Mkoa wa Singida Dk.Binilith Mahenge alisema  Mwenge huo utakimbizwa kwa muda wa siku tano  katika wilaya tano kwa kuanzia na Wilaya ya Iramba na utahitimisha mbio zake Julai 24/2021 ambapo utakabidhiwa Mkoa wa Dodoma.

Alisema Mwenge wa Uhuru utakapokuwa Mkoani hapa  utakimbizwa jumla ya kilometa 642.3, utapitia jumla ya miradi 55 inayohusu TEHAMA, Elimu, Afya, Mazingira, Maji, Biashara, Barabara na Programu za Rushwa, Malaria, mapambano dhidi ya Dawa za Kulevya,VVU/UKIMWI na Lishe.Miradi 9 itazinduliwa, miradi 2 itafanyiwa ufunguzi, miradi 6 itawekwa jiwe la msingi, miradi 36 itakaguliwa na Miradi 2 itatembelewa. 

Alisema miradi yote itakayopitiwa na mwenge huo itakuwa na thamani ya Sh. 8,182,219,653.99 ambapo alitoa mchanganuo wake kuwa nguvu za wananchi ni Sh. 1,957,623,652.58, Halmashauri Sh. 69,630,194.42, Serikali Kuu Sh.4,627,922,247.27 na Wahisani sh.1,527,043,559.72.

Alisema  ujumbe wa Mwenge wa Uhuru mwaka2021 ambao utatolewa maeneo mbalimbali ya Wilaya za Mkoa wa Singida ni “Matumizi Sahihi ya TEHAMA” chini ya Kauli Mbiu inayosema  TEHAMA ni Msingi wa Taifa Endelevu;Itumike kwa Usahihi na Uwajibikaji.

Dk. Mahenge alisema Mkoa wa Singida umekuwa ukiamini kuwa TEHAMA ni msingi wa maendeleo endelevu, kwani matumizi sahihi ya miundombinu na mifumo ya TEHAMA yamewezesha kurahisisha mawasiliano, ukusanyaji na kuongeza mapato ya Serikali, kudhibiti matumizi ya Fedha za Umma, kuongeza uwazi na uwajibikaji katika kuwatumikia Wananchi, kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi,kurahisisha taratibu za manunuzi ya Umma na kuondoa mianya ya rushwa na ubadhilifu, urahisi kwa wananchi kulipia ankara mbalimbali, kurahisisha na kuwezesha upatikanaji wa Takwimu mbalimbali kwa usahihi na kwa wakati.

" Kwa kutambua faida hizi zitokanazo na matumizi sahihi ya TEHAMA, Mkoa wa Singida umeendelea kusimamia mifumo ya TEHAMA zaidi ya 30 inayotumika katika Mamlaka za Serikali za Mitaa, Sekretarieti ya Mkoa pamoja na Taasisi mbalimbali zilizopo ndani ya Mkoa wa Singida," Mahenge.

Alitaja baadhi  ya Mifumo ya TEHAMA inayotumika katika Mamlaka za Serikali za Mitaa na Taasisi nyingine ni pamoja na mifumo ya fedha ya ukusanyaji wa mapato na matumizi ambayo ni ‘Local Government Revenue Collection Information System (LGRCIS)’, ‘e-Revenue Management System’ unaotumiwa na TARURA.  Mifumo ya uhasibu Serikalini (MUSE)naFFARS. 

Aidha Dk. Mahenge alitaja mfumo mwingine kuwa ni wa TEHAMA wa TANEPs unahusika na Manunuzi ya Umma, Mfumo GoTHOMIS unatumika kudhibiti makusanyo ya vituo vya kutolea huduma za Afya pamoja na upotevu wa dawa na vifaa tiba, mfumo waTEHAMA wa ukusanyaji wa takwimu za Kilimo (ARDS), mifumoya PREM, PREMs, School Information System (SIS) na Annual School Sensor (ASC) kwaajili ya kupata takwimu sahihi za elimu na mfumo wa (HCMIS)) kwaajili ya Taarifa za kiutumishi na Mishahara.


Share To:

Post A Comment: