Mbunge wa Singida Mashariki Miraji Mtaturu, akizungumza na Wananchi wa Kijiji cha Matongo  wakati akiongoza harambee ya ujenzi wa Shule ya Sekondari ya Matongo iliyofanyika Kata ya  Ikungi mkoani Singida juzi.
Wanafunzi wakiongoza  msafara wa Mbunge wa Singida Mashariki Miraji Mtaturu wakati alipofika kukagua ujenzi wa madarasa ya Shule ya Msingi ya  Kitongoji cha Mwau.
Mbunge wa Singida Mashariki Miraji Mtaturu akizungumza na Wananchi wa Kitongoji cha Mwau.
Mbunge wa Singida Mashariki Miraji Mtaturu, akikagua ujenzi wa Shule ya Msingi ya Mbughantigha.


Harambee ikiendelea.
Wananchi wakiwa kwenye harambee hiyo.
Wananchi wakiwa kwenye harambee hiyo.
Harambee ikiendelea.
 Diwani wa Kata ya Ikungi itakapojengwa shule hiyo, Abel Nkuwi akizungumza kwenye harambee hiyo.
Mwalimu Yesaya Benjamin  akizungumza kwenye harambee hiyo.
Harambee ikiendelea.
Mwenyekiti wa Kijiji cha Matongo, Abubakari Selemani, akizungumza kwenye harambee hiyo.
Burudani zikitolewa kwenye harambee hiyo.
Harambee ikiendelea.
Diwani wa Viti Maalumu, Magreth Philemon akizungumza kwenye harambee hiyo wakati akichangia.
Askari Polisi Justine Dominic kutoka Kituo cha Polisi cha Kijiji cha Matongo akichangia Sh.50,000 kwenye harambee hiyo.
Harambee ikiendelea.
Harambee ikiendelea.
Mbunge wa Singida Mashariki Miraji Mtaturu, akipokea saruji iliyotolewa na vikundi mbalimbali.


Dotto Mwaibale Singida


MBUNGE wa Singida Mashariki Miraji Mtaturu ameendesha harambee ya ujenzi wa Shule ya Sekondari ya Kijiji cha Matongo iliyopo  wilayani Ikungi mkoani Singida ambapo zaidi ya Sh..10 milioni zilipatikana.

Mtaturu ambaye alikuwa mgeni rasmi alitoa mifuko ya saruji 100 kwa ajili ya kuanza kufyatua matofali ili ujenzi huo uanze mara moja.

Katika harambe hiyo  wananchi na wadau mbalimbali wa elimu walishirikishwa ambapo licha ya kupatikana fedha hizo pia ilipatikana mifuko ya saruji 259, malori ya mchanga 15, bati bando mbili, matofali 1000 na matela ya mchanga 10.

Fedha na michango hiyo inakwenda kuanza kujenga madarasa  na kutatua adha ya wanafunzi wa kijiji hicho ambao wanatembea umbali wa kilometa 13 kwenda kusoma  Shule ya Sekondari ya Ikungi Mchanganyiko jambo linalowasababishia  kushindwa kuhudhuria vizuri masomo yao.

Akizungumza juzi katika harambe hiyo Mtaturu aliwaambia wananchi  wa kijiji  hicho kuwa elimu ndio mkombozi na kila mtu anawajibu wa kuchangia ambapo aliwahakikishia kuwa Serikali itaendelea kuboresha miundombinu ya shule na kutoa elimu bure bila malipo kuanzia shule ya awali hadi kidato cha nne.

Alisema Serikali itaendelea kujenga miundombinu ya elimu, kuongeza idadi ya walimu na kujali maslahi yao hivyo aliwaomba wafanye kazi kwa bidii kwani Rais Samia Suluhu Hassan anawapenda watumishi wote hapa nchini.

Mtaturu alitumia nafasi hiyo kuwaeleza wananchi hao kuwa Serikali imepanga kuboresha miundombinu ya barabara katika jimbo hilo la Singida Mashariki ambapo nje ya bajeti yake ya mwaka huu imetoa Sh 1.5 Bilioni kwa kazi hiyo.

Akizungumzia sekta ya afya alisema  Serikali  katika bajeti yake ya mwaka huu imeongeza fedha ukilinganisha na ya mwaka wa fedha uliopita.

Alisema serikali mbali ya kuboresha miundombinu ya barabara itapeleka umeme na maji katika maeneo yote ya jimbo hilo kikiwemo kijiji hicho cha Matongo.

Katika hatua nyingine Mitaturu amechangia mabati 200 kwa ajili ya kupaua madarasa mawili ya shule shikizi ya kitongoji cha Mwau ambayo yamejengwa kwa nguvu za wananchi.

 Kukamilika kwa madarasa hayo kutawapunguzia changamoto watoto wa eneo hilo kutembea umbali wa kilometa saba kila siku kwenda Matongo kwa ajili ya kupata elimu.

Akizungumza na wananchi wa Kitongoji cha Mbughantigha wakati akikagua ujenzi wa madarasa mawili yaliyojengwa kwa nguvu zao aliwataka wajenge madarasa mengine mawili na nyumba ya mwalimu ili shule hiyo iweze kupata usajili.

Mtaturu alisema wametoka kwenye Bajeti ya Serikali ya Awamu ya sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassan ambayo imelenga kuwaletea wananchi maendeleo. 

"Tunamshukuru sana Rais kwa kuonyesha upendo mkubwa kwa watanzania tumuunge mkono," alisema Mtaturu.

Diwani wa Kata ya Ikungi Abel Nkuwi alisema wanadhamira ya kujenga shule hiyo ya sekondari katika kijiji hicho ili kuwasaidia watoto ambao wanatembea umbali mrefu kwenda Ikungi kupata elimu.

Alisema kwa utangulizi ujenzi wa shule hiyo utagharimu sh.72 milioni na kuwa wamepanga kila mwananchi mwenye uwezo katika eneo hilo achangie sh.15,000 ambapo wanatarajia kupata Sh. Milioni 48 hivyo kuanza mara moja kazi ya ujenzi huku fedha zingine zikitokana na harambee hiyo na vyanzo vingine.

Mwanafunzi Nani Aley wa kidato cha pili anayetoka katika kijiji hicho kwenda kusoma Sekondari ya Ikungi Mchanganyiko alisema kukamilika kwa ujenzi wa shule hiyo kutawaondolea changamoto ya kutembea kila siku kwenda shuleni na kuwapunguzia mzigo wa gharama wazazi wao kwa kuwapangia nyumba za kuishi wakiwa shuleni Ikungi.

Aley alitumia nafasi hiyo kumshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuwapa elimu bure pasipo malipo pamoja na Mbunge wao Mtaturu, Diwani wa Kata hiyo na viongozi wote na wananchi kwa kuanza mchakato wa ujenzi wa sekondari katika kijiji hicho.

Share To:

Post A Comment: