MENEJA wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Mkoani Tanga (NHIF) Ally Mwakababu kushoto akisisitiza jambo kwa Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara Exaud Kigahe (MB) wakati alipotembelea Banda lao lililopo kwenye maonyesho ya Biashara ya 8 yanayoendelea kwenye viwanja vya Mwahako Jijini Tanga
Meneja wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Mkoani Tanga (NHIF) Ally Mwakababu kushoto akimsikiliza kwa umakini Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara Exaud Kigahe (MB) wakati alipotembelea Banda lao lililopo kwenye maonyesho ya Biashara ya 8 yanayoendelea kwenye viwanja vya Mwahako Jijini Tanga
Meneja wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Mkoani Tanga (NHIF) Ally Mwakababu akizungumza na waandishi wa habari ambao hawapo pichani namna walivyojipanga kutoa elimu kwa wananchi juu ya umuhimu wa kujiunga na bima ya Afya

Meneja wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Mkoani Tanga (NHIF) Ally Mwakababu katika akiwa kwenye picha ya pamoja na watumishi wa mfuko huo kwenye banda lao kulia ni Afisa Matekelezo wa NHIF mkoa wa Tanga Macrina Clemence


NA OSCAR ASSENGA, TANGA.

MENEJA wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Mkoani Tanga (NHIF) Ally Mwakababu amewahamasisha wakazi wa mkoa huo kuchangamkia fursa ya kujiunga na mfuko huo ili kuweza kujihakikishia kupata huduma za matibabu wanapoungua na hivyo kuwaondolea wasiwasi akiugua itakuwaje.

Mwakababu aliyasema hayo wakati akiwa eneo la Mwahako Jijini Tanga kunakoendelea maonyesho ya nane ya Biashara ambapo alisema kuwa na kadi ya bima ni kuwa na daktari hivyo inakusaidia kukuondolea wasiwasi pindi unapougua huku ukiwa hauna fedha.

Alisema hivyo wananchi wanapaswa kutambua umuhimu wa kujiunga na mfuko huo na kuweza kunufaika na huduma mbalimbali za kimatibabu pindi wanapougua

Meneja huyo alisema wameshiriki kwenye maonyesho hayo ya biashara ya TCCIA kwao wanaamini bima ya afya kwa wote serikali ya awamu ya sita inapambana kuhakikisha watu wanajiunga na bima ya afa badala ya kusubiri kupata matibabu kulipia.

“Kwa hiyo ndio maana tupo hapa kutoa elimu kwa wanachama na ushauri wa afya zao kwa kupima uzito,presha,sukari na kushauri mwenendo mzuri wa kula na kuwaeleza umuhumi wa kujiunga na bima”Alisema

Alisema pia ikiwemo Toto Afya Kadi na makundi mbalimbali ambayo serikali imeyaweka kwenye mpango ambao ni wakulima kupitia Amcos zao,waandishi wa habari katika eneo lao walipe laki moja,makundi ya wavuvi,warina asali na watu binafasi wa na vifurushi mbalimbali ikiwemo najali,timiza.

Hata hivyo aliwaomba wananchi wajiunge na wafike na kuchangmkia fursa za kujiunga na mfuko huo kwani kuwa na kadi ya bima inakuhakikishia kupata matibabu .

Mwisho.

Share To:

TANGA RAHA BLOG

Post A Comment: