Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Ndg. Daniel Chongolo amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Watu wa Korea  nchini Tanzani Mhe. Kim Yong Sung.


Mazungumzo hayo yamefanyika leo tarehe 9 Juni, 2021 katika Ofisi za CCM Makao Makuu Dodoma.


Katika mazungumzo hayo, pamoja na mambo mengine Balozi huyo amekutana na Katibu Mkuu kwa lengo la utambulisho na kuendeleza Ushirikiano na Urafiki wa Kihistoria uliopo kati ya Chama Cha Mapinduzi na Chama Tawala cha Wafanyakazi Cha  Korea Kaskazini (Workers Party Of Korea).


Kikao hicho kimehudhuriwa na Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, Siasa na Uhusiano wa Kimataifa Ndg. Ngemela Lubinga.


Huu ni Muendelezo wa Katibu Mkuu kukutana na Mabalozi wa nchi mbalimbali wanaoziwakilisha nchi zao hapa Tanzania kuendelea kutambulishana na kuendeleza uhusiano mzuri uliopo baina ya Tanzania na nchi nyingine, ambapo mwishoni mwa mwezi Mei mwaka huu alikutana na Balozi wa China nchini Tanzania.

Share To:

msumbanews

Post A Comment: