Naibu Waziri wa Uchukuzi Mhe. Mwita Waitara akifungua kikao wakati alipokutana na Chama cha wamiliki wa Mabasi hapa nchini TABOA kwa lengo kusikiliza kero mbalimbali zinazowakumba katika biashara zao kilichofanyika leo May 3,2021 jijini Dodoma.
Naibu Waziri wa Uchukuzi Mhe. Mwita Waitara akifungua kikao wakati alipokutana na Chama cha wamiliki wa Mabasi hapa nchini TABOA kwa lengo kusikiliza kero mbalimbali zinazowakumba katika biashara zao kilichofanyika leo May 3,2021 jijini Dodoma.
Mjumbe wa Chama cha Wamiliki wa Mabasi (TABOA) Elinas Kitua,akitoa maoni wakati wa kikao na Naibu Waziri wa Uchukuzi Mhe. Mwita Waitara pamoja na Chama cha wamiliki wa Mabasi hapa nchini TABOA kwa lengo kusikiliza kero mbalimbali zinazowakumba katika biashara zao kilichofanyika leo May 3,2021 jijini Dodoma.
Mmiliki wa Mabasi ya Arizona Coarch ,Yahaya Massare,akitoa kero zake ambazo zinamkutana katika biashara zake za usafiri w Mabasi wakati walipokutana na kikao ambacho kilikuwa lengo la kusikiliza kero mbalimbali zinazowakumba katika biashara zao kilichofanyika leo May 3,2021 jijini Dodoma.
Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Wamiliki wa Mabasi (TABOA) ambaye pia ni Mmiliki wa Mabasi ya Isagilo Express kanda ya Ziwa Bw.Eliah Peter,akizungumza kwenye kikao cha Naibu Waziri wa Uchukuzi Mhe. Mwita Waitara na Wamiliki wa Mabasi hapa nchini TABOA wenye lengo la kusikiliza kero mbalimbali zinazowakumba katika biashara zao kilichofanyika leo May 3,2021 jijini Dodoma.

Mmiliki wa Mabasi ya Super/Selons Express Francis Sengo,akizungumza kwenye kikao cha Naibu Waziri wa uchukuzi Mhe. Mwita Waitara na Wamiliki wa Mabasi hapa nchini TABOA wenye lengo la kusikiliza kero mbalimbali zinazowakumba katika biashara zao kilichofanyika leo May 3,2021 jijini Dodoma.

Naibu Waziri wa Uchukuzi Mhe. Mwita Waitara ,akizungumza mara baada ya kusikiliza kero za Wamiliki wa Mabasi hapa nchini TABOA Kikao ambacho kilikuwa na lengo la kusikiliza kero mbalimbali zinazowakumba katika biashara zao kilichofanyika leo May 3,2021 jijini Dodoma.


Baadhi ya washiriki wa Kikao wakimsikiliza Naibu Waziri wa uchukuzi Mhe. Mwita Waitara(hayupo pichani) wakati ,akizungumza na Wamiliki wa Mabasi hapa nchini TABOA Kikao ambacho kilikuwa na lengo la kusikiliza kero mbalimbali zinazowakumba katika biashara zao kilichofanyika leo May 3,2021 jijini Dodoma.


Na.Alex Sonna,Dodoma

Serikali imewahakikishia chama cha wamiliki wa mabasi hapa nchini TABOA kuwa itahakikisha inatatua na kumaliza changamoto zote ambazo ni kikwazo kwa wafanyabiashara hao ikiwamo mfumo mpya wa ukatishaji tiketi mtandao.

Huku ikizitaka taasisi zinazosimamia usafirishaji kuhakikisha wanatatua kero na malalamiko yanayohusu wasafirishaji kwa wakati pindi zinapofika ofisini kwao.

Hayo yamebainishwa jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Uchukuzi Mhe. Mwita Waitara alipokutana na chama cha wamiliki wa mabasi hapa nchini TABOA kwa lengo kusikiliza kero mbalimbali zinazowakumba katika biashara zao.

Ambapo amesema Serikali inania nzuri ya kuhakikisha wafanyabiashara wa mabasi wanafanyakazi bila ya kuwa na vikwazo kwani wao ni moja ya sekta muhimu ya kuchocheo uchumi hapa nchini.

“Serikali inania nzuri sana na lengo lake ni kuhakikisha ninyi mnafanyakazi kwa uhuru ndio maana leo nimekuja hapa niwasikilize nini kikwazo kwenu kwa kuwa sekta yenu ni muhimu sana kuwasafirisha wananchi ili nao walipe kodi nchi ijiendeshe” amesema Waitara.

Ameongeza kuwa “Nimewasikiliza kero zenu zote niwahakikishie tu kero zenu zote zitafanyiwa kazi hata hii kelele ya muda mrefu ya tiketi mtandao tutalifanyia kazi kwa kuwa taarifa ni kwamba mfumo unafanyiwa marekebisho bado haujawa rasmi utaboreshwa” amesema.

Ameitaka Mamlaka ya udhibiti wa usafiri ardhini LATRA kuhakikisha kero, changamoto na malalamiko mbalimbali ya TABOA yanafanyiwa kazi haraka pia wajenge utaratibu wa kusikiliza kero na kuzijibu kwa wakati ili sekta ya usafirishaji iweze kukua hapa nchini.

“Nimepata ushahidi hapa kwa barua mbalimbali kutokujibiwa na mimi mwenyewe shahidi kuna taarifa yangu niliomba haijafanyiwa kazi pia kuna mbunge mwenzangu katuma maombi ya kubadilisha tu rout(njia) lakini mpaka leo haijajibiwa shida ni nini” amesema.

Aidha Mhe. Waitara amesema atahakikisha anawakutanisha LATRA na TABOA ili malalamiko yao yote yaweze kujibiwa moja kwa moja ili changamoto hizo ziweze kuondoka kabisa sambamba na hilo ili LATRA waweze kuwapitisha katika mfumo huo ili TABOA waweze kuelewa namna mfumo huo unavyofanyakazi na malengo ya kuanzishwa kwake.

Awali wajumbe wa TABOA wameiomba serikali kuitazama upya LATRA na muundo wake kwani kanuni zao nyingi si rafiki kwao zinaweza kupelekea kupoteza mitaji yao kwa kufilisika kutokana na makato mengi katika biashara hiyo.

Pia wamesema mfumo wa tiketi mtandao wao ndio waanzilishi lakini sasa imekuwa tofauti na malengo ya kuanzishwa kwake kwa sasa imekuwa mwiba kwao hasa baada ya kutakiwa kujaza flot kabla ya kuanza kufanyakazi na kuwa na utitili wa makato tofauti na mashine nyingine za kutolea lisiti.


Share To:

TANGA RAHA BLOG

Post A Comment: