Baada ya kukabidhiwa wanaviangalia vipima Oxijeni hivyo
MBUNGE wa Viti Maalumu (CCM) Kundi la 
Asasi za Kiraia (NGOs) Mh Neema Lugangira na rais wa Baraza la 
Watanzania wanaoishi Marekani (DICOTA) leo wamekabidhi msaada wa Vipima 
Oxijeni (Pluse Oximeters) 108 kwa Ofisi ya Rais TAMISEMI kwa ajili ya 
Vituo vya Afya kutoka Mikoa 11 ikiwa ni mchango wao katika kuthamini 
juhudi za Serikali katika kuimarisha Afya za Watanzania.
Msaada
 huo umepokelewa na Naibu Waziri wa Ofisi ya Rais TAMISEMI 
anayeshughulikia Masuala ya Afya; Mhe Dkt Festo Dugange  ambapo vifaa 
hivyo vitagawiwa katika mikoa ya Dar-es Salaam, Dodoma, Kigoma, Kagera, 
Kilimanjaro, Arusha, Tanga, Ruvuma, Mbeya, Lindi na Njombe.
Akizungumza
 baada ya kukabidhi msaada huo wa vifaa, Mbunge wa NGOs Tanzania Bara, 
Mhe Neema Lugangira alimshukuru Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI, 
Mhe Ummy Mwalimu kwa ushirikiano mkubwa aliowapatia katika kufanikisha 
shughuli hiyo ya leo.
Mbunge
 Neema Lugangira alisema pia wanashukuru Dkt Grace Maghembe, Naibu 
Katibu Mkuu na Dkt Ntuli Kapologwe, Mkurugenzi wa Idara ya Masuala ya 
Afya, Lishe kwa ushirikiano wao mkubwa ambao wamekuwa wakiendelea 
kuwapatia.
“Sisi 
tunamshukuru sana Waziri wa Nchi OR TAMISEMI Mhe. Ummy Mwalimu, kuridhia
 kupokelewa kwa msaada huu, ambao umepokelewa na Naibu Waziri, Dkt. 
Festo Dugange. Mimi kama Mbunge nitaendeleza jitihada hizi kwa niaba ya 
Serikali ili lengo la kuimarisha Afya ya Mtanzania iweze kutimia,” 
Alisema Lugangira.
Awali 
akizungumza wakati akiipokea msaada huo wa vifaa tiba ambavyo vinatumika
 kupima kiasi cha Oxijeni katika mwili wa mwanadamu, Naibu Waziri Ofisi 
ya Rais TAMISEMI anayeshughulikia afya, Mhe Dkt. Festo Dugange 
amewapongeza Watanzania hao waishio Marekani kwa kuthamini juhudi za 
Serikali ya Nchi yao za kujenga na kukarabati miundombinu mbalimbali ya 
afya nchini.
Alisema ili 
kuhakikisha kuwa jukumu hilo linatekelezwa kikamilifu, Naibu Waziri 
ameongeza kuwa katika bajeti ya mwaka 2021/22 serikali imetenga shilingi
 bilioni 65 kwa ajili ya kununulia dawa na vifaa tiba.
“Serikali
 imefanya kazi kubwa ya ujenzi wa Miundombinu na katika mwaka wa fedha 
2021/22 tumeweka kwenye bajeti ya dawa na vifaa tiba kama hivi na 
vingine kiasi kinachofikia Bil.65, hivyo kwa jitihada hizi za wadau hawa
 na wengine wote watakao kuja hapo baadaye ni ishara kwamba lengo letu 
la kuweka vitendanishi na dawa litatimia,” amesema Mhe Naibu Waziri Dkt.
 Dugange.
Akiongea kwa 
niaba ya Watanzania waishio nchini Marekani, rais wa DICOTA, Dkt. Frank 
Minja, amesema, wanaona fahari ya kuchangia vifaa hivyo ambavyo 
vitakwenda kugawiwa kwenye ngazi ya Hospitali za Wilaya na kutumika na 
watanzania wenzao na kuahidi ni mwanzo ambapo wanatarajia kufanya mengi 
zaidi kwa kushirikiana na Serikali na Mbunge Lugangira katika Sekta hii 
ya Afya.
Naye Naibu 
Katibu Mkuu Ofisi ya Rais TAMISEMI anayeshughulikia Afya Dkt. Grace 
Magembe, amesema kuwa atahakikisha kuwa vifaa vilivyopokelewa vinatunzwa
 ili viweze kudumu kwa muda mrefu.
Hafla
 ya kukabidhi vifaa tiba ilifanyika Makao Makuu ya Ofisi ya Rais 
TAMISEMI jijini Dodoma na kuhudhuriwa pia na Mkurugenzi wa Huduma za 
Afya, Lishe na Ustawi wa Jamii kutoka Ofisi ya Rais TAMISEMI Dkt. Ntuli 
Kapologwe na Katibu Mtendaji wa Tume ya Utumishi wa Walimu Paulina 
Mkwama.
MWISHO



Post A Comment: