Mbunge wa Jimbo la Singida Mashariki Miraji Mtaturu akishiriki uchimbaji wa msingi wa Shule ya Msingi ya Mbwanjiki  ambapo pia alitoa  msaada wa vifaa vya ujenzi.

Mbunge wa Jimbo la Singida Mashariki Miraji Mtaturu akikabidhi mifuko ya saruji,
Mbunge wa Jimbo la Singida Mashariki Miraji Mtaturu akiwa na wananchi wakati wa utoaji wa msaada huo.
Mbunge wa Jimbo la Singida Mashariki Miraji Mtaturu akisshhiriiki kubeba ma4ofari.
Mbunge wa Jimbo la Singida Mashariki Miraji Mtaturu akikabidhi saruji na mabati.
Mbunge wa Jimbo la Singida Mashariki Miraji Mtaturu akikagua ujenzi wa madarasa ya Shule ya Msingi ya Mbwanjiki.


Na Dotto Mwaibale, Ikungi


MBUNGE wa Jimbo la Singida Mashariki Miraji Mtaturu ameshiriki shughuli za maendeleo katika Jimbo hilo ikiwemo utoaji wa msaada wa vifaa vya ujenzi.

Akizungumza na waandishi wa habari wakati akishiriki ujenzi huo alisema ameanza kwa  kuchimba msingi,kusogeza tofali na kukabidhi mifuko 30 ya saruji katika Shule ya Msingi ya Mbwanjiki ili kuendeleza ujenzi huo uliokwama kwa takribani miaka 30.

"Kukamilika kwa ujenzi wa shule hiyo kutaondoa changamoto ya wanafunzi kutembea umbali mrefu na msongamano katika shule wanazosoma za Ikungi,Ighuka na Matongo". alisema Mtaturu.

Mtaturu alitumia nafasi hiyo kuwapongeza walimu kwa jitihada zao za kufundisha watoto na kuwaomba wazazi kuendelea kushirikiana na walimu ili kuongeza ufaulu.

“Najua walimu wetu mnapambana ili kuhakikisha watoto wetu wanafaulu na shule yetu inakuwa katika nafasi nzuri,niwatie moyo kuwa nipo pamoja na ninyi, nimejivika joho la kuwa champion wa elimu katika jimbo hili,ahadi hii nitaitekeleza kwa vitendo.”alisema.Mtaturu 

mbali na kutembelea shule hiyo pia alifanikiwa kufika Shule ya Msingi Minyinga kuangalia athari ya mvua zilizoezua paa za madarasa na kuchangia saruji mifuko 20 ,bati 30 na matofali 500.

Akitoa msaada huo Mtaturu ameziomba kamati za shule kuweka mkazo kwenye lishe mashuleni ili kuwafanya watoto wawe watulivu na kuzingatia masomo ikiwa ni jitihada za kukuza taaluma.

Aidha Mtaturu aliishukuru Serikali ya awamu ya tano chini ya Rais Dkt. John Magufuli  kwa kuendelea kutoa elimu bila malipo na kuleta fedha za miradi ya maendeleo ikiwemo miundombinu katika shule za msingi na sekondari.

 Alisema kazi hiyo kubwa inayofanywa na Serikali iwe chachu katika kuhakikisha kila mmoja anatimiza jukumu lake ili lengo la Rais Magufuli liweze kufikiwa.

Kwa upande wao Diwani wa Kata ya Ikungi Abely Nkuwi na wa Kata ya Makiungu John Mathias wameunga mkono jitihada za mbunge na kuchangia tofali 200 huku diwani wa viti maalum Zainab Ntui akichangia sh  100,000.

Ziara ya mbunge huyo imemfikisha pia katika ujenzi wa daraja lililopo Kata ya Ntuntu linalojengwa na Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (Tarura ) ambalo litasaidia kuondoa kero ya kukatika kwa mawasiliano pindi mvua inaponyesha.

Daraja hilo linajengwa kwa gharama ya zaidi ya sh. milioni 90, madaraja madogo pamoja na matengenezo ya barabara ya Mungaa -Ntuntu hadi Mang'onyi ambapo shughuli zote hizo zinagharimu zaidi ya  sh. milioni 142.

Share To:

Post A Comment: