FAINALI
za mashindano ya urembo nchini maarufu kama 'Miss Tanzania'
zinatarajiwa kuhitimishwa Desemba 5, mwaka huu katika ukumbi wa
kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es Salaam huku mgeni
rasmi akitarajiwa kuwa Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Dkt. Tulia Ackson.
Akizungumza na waandishi wa habari
leo jijini Dar es Salaam Mkurugenzi wa Kampuni ya 'The Look'
inayosimamia na kuandaa mashindano hayo Basila Mwanukuzi amesema, hiyo
ni mara ya tatu mfululizo kwa Kampuni hiyo kuandaa mashindano hayo,
ambayo kwa sasa yanakwenda na kauli mbiu ya "Urembo ni heshima."
"Dkt.
Tulia amethibitisha kuwa mgeni rasmi wa shindano hilo na tunaelewa kuwa
Naibu spika ni mwanamichezo, mpenda sanaa na kinara katika shughuli
zinazoweka kipaumbele katika kusaidia jamii na amekuwa akifuatilia kwa
karibu mashindano haya ambayo yanaendeshwa kwa malengo mashindano ya
kidunia yaani 'Beauty with Purpose'." Ameeleza.
Amesema, katika
mashindano hayo jumla ya walimbwende 20 kutoka Mikoa mbalimbali ya
Tanzania wamefuzu katika fainali hizo za kumsaka Miss Tanzania.
Basila
amesema, licha ya changamoto ya mlipuko wa ugonjwa wa Korona mwanzoni
mwa mwaka, mwitikio ulikuwa mkubwa kwa warembo wengi, wenye vigezo
kujitokeza kushiriki mashindano hayo na tayari warembo 20 walioingia
katika fainali hizo wana miradi yao ya kusaidia jamii (BWAP) yaani
'Beauty with Purpose Project' ambayo zitashindaniwa na kumpata mshindi.
Post A Comment: