Na Shamimu Nyaki-WHUSM, Dodoma

Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Hassan Abbasi

ameiagiza Idara ya Maendeleo ya Michezo nchini kukutana na Wadau wa sekta hiyo

wakiwemo Mashirikisho na Vyama vya Michezo ili kubadilishana utaalamu wa namna

ya kuendesha michezo kwa pamoja na kutoa ushauri wa kisera kwa wadau hao.

Dkt. Abbasi ametoa maagizo hayo leo Novemba 21, 2020 Jijini Dodoma katika kikao

watumishi wa Idara hiyo ambapo amewataka kusimamia kikamilifu Sekta ya Michezo

ambayo inaendelea kuletea heshima Taifa.


"Ni lazima mkutane na Wadau wenu ili mjue wana mawazo gani katika sekta hii na nyie

mtoe ushauri wa kitaalamu ambao utaleta tija. Ni lazima muwaeleze wadau Sera ya

Michezo inasemaje kwa sababu nyie ndio mnaoisimamia sekta hii ", alisema Dkt.

Abbasi.


Aidha, Katibu Mkuu huyo ameitaka Idara hiyo kuhakikisha kila Shirikisho au Chama cha

michezo vinawasilisha Mpango Mkakati wake katika Baraza la Michezo la Taifa (BMT)

ambao pamoja na mambo mengine, utaonyesha kalenda ya mwaka katika ligi za kitaifa,

kimataifa pamoja na timu ya Taifa . Lengo likiwa ni kuhakikisha kunakuwepo na uelewa

wa pamoja kwa wadau wote utakaoleta mafanikio zaidi katika sekta hiyo.

Dkt. Abbasi amesema kuwa Taifa lazima liwe na ushiriki wa mashindano ya michezo

ambao utaleta tija, hivyo Idara hiyo ina jukumu la kuhakikisha mashindano yote ambayo

nchi inashiriki katika ngazi mbalimbali yanakua na manufaa, ameongeza kuwa katika

mashindano mbalimbali ikiwemo Olympiki lazima kama nchi kujua aina ya michezo ya

kushiriki.


Vilevile, Dkt. Abbasi ameongeza kuwa mashindano ya UMITASHUMTA na UMISETA

ni mashindano ambayo yanapaswa kupewa kipaumbele kwa kuwa yanazalisha vipaji

vingi vya michezo mbalimbali nchini. Hivyo, Idara ya Michezo ina jukumu la kusimamia

mashindano hayo kwa kushirikiana na wadau wengine ikiwemo TAMISEMI na Wizara

ya Elimu ili vijana wanaofanya vizuri waendelezwe kupitia Chuo cha Maendeleo ya

Michezo Malya pamoja na sehemu nyingine.


Kwa upande mwingine Katibu Mkuu huyo amesema kuwa ushirikiano kati ya Tanzania

Bara na Zanzibar katika sekta ya Michezo unaendelea kuimarika ikiwemo kuimarisha

Kombe la Mapinduzi.


;Muungano wetu ni muhimu na Kombe la Mapinduzi ni moja ya njia ya kutuunganisha

na kuimarisha Muungano wetu, hivyo nitoe rai kwa Vilabu kupeleka timu bora katika

mashindano hayo"alisema Dkt.Abbasi.


Akiongelea kuhusu miuondombinu ya michezo ikiwemo ujenzi wa viwanja, Dkt. Abbasi

ameeleza kuwa Serikali inaendelea kuwekeza na matarajio ni kuwa na viwanja bora vya

michezo nchini na tayari Ujenzi wa Uwanja wa Dodoma umefikia hatua nzuri.

Share To:

Post A Comment: