Na. Angela Msimbira OR-TAMISEMI
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mhe.  Selemani Jafo amesema uwekezaji mkubwa uliofanywa katika sekta ya elimu na serikali ya awamu ya tano chini ya Rais Dk John Magufuli ndio siri iliyopelekea shule nane za serikali kuingia kwenye kumi bora katika matokeo ya kidato cha sita 2020.

Ameyasema hayo jana ofisini kwake Jijini Dodoma wakati akiongea na waandishi wa habari kuhusu ufaulu wa Shule za sekondari zinazomilikiwa na Serikali katika matokeo ya kidato ya sita.

Amesema katika kipindi cha miaka mitano Serikali imeendelea kufanya vizuri katika Sekta ya Elimu ambapo kwenye matokeo yaliyotangazwa leo tarehe 21/08/2020  ufaulu umeongezeka kwa wanafunzi wa kidato cha sita kutoka  asilimia 98 kwa mwaka 2019 hadi kufikia asilimia 99.51 kwa mwaka.

Amesema kuwa katika matokeo hayo shule za Serikali nane zimeweza kuingia katika  shule kumi bora kwa mara ya kwanza zikiwemo shule za kata 3 ambazo ni Kasimiri, Mwandeti na Dareda.

Amezitaja shule za Serikali zilizoshika nafasi kumi bora kuwa ni Mzumbe, Shule ya wasichana Tabora, shule ya wavulana Tabora, Iiliboru na  Kibaha

“Zamani ufaulu wa shule za Serikali ulikuwa mdogo  kiasi kwamba wazazi walikuwa hawapendi kuwapeleka watoto wao kusoma katika shule hizo wanapochaguliwa kujiunga na shule hizo, lakini sasa shule hizo zimekuwa na ufaulu mkubwa na kuwa tegemeo  kwa wazazi kuwapeleka watoto wao” amesema Waziri Jafo

Waziri Jafo anafafanua kuwa  uwekezaji uliofanywa na Serikali ya awamu ya Tano chini ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli umeleta mabadiliko makubwa katika eneo la taaluma nchini

Aidha. Jafo amewashukuru waalimu, maafisa elimu Mikoa na Wilaya kwa usimamizi uliotukuka wa kuhakikisha  vijana wa kidato cha sita wanafaulu  vizuri na kuliongezea taifa sifa katika suala zima la sekta ya Elimu.

Amewapongeza Wanafunzi wote wa kidato cha Sita kwa kusoma kwa bidi na kupata ufaulu mzuri japokuwa kulikuwa na  changamoto ya ugonjwa wa CORONA nchi ya Tanzania bado waliweka juhudu katika masomo na kufaulu mitihani yao vizuri.

Waziri Jafo anaendelea kusema kuwa Serikali imetumia kiasi cha shilingi trilioni 1.09 katika suala zima la utoaji wa elimu bila malipo ambayo imehamasisha  sekta ya Elimu nchini,pia kiasi cha shilingi milioni 588 kwa ajili ya  ujenzi wa miundombinu  jambo hili limesaidia kuongeza idadi ya ufaulu wa wanafunzi.

Sambamba na hilo amesema kuwa Serikali imeweza kuongeza idadi ya waalimu  kwa lengo la kuongeza rasilimali ambao  watasaidia kupeleka elimu juu zaidi hali ambayo inapelekea kuongeza ufaulu zaidi nchini.

"Matokeo hayo yameonyesha pia wanafunzi waliopata daraja la kwanza hadi la tatu ni asilimia 97.74, haya ni mafanikio makubwa,malengo yetu yalikuwa kuingiza shule sita za serikali kwenye kumi bora lakini tumeingiza shule nane,huu ni ufaulu uliozidi viwango" amesema Waziri Jafo.
Share To:

msumbanews

Post A Comment: