Klabu ya simba, Jana Agosti 30 iliibuka na ushindi wa mabao 2-0 mbele ya Namungo FC na kufanikiwa kutwaa taji la Ngao ya Jamii kwenye mchezo uliochezwa Uwanja wa Sheikh Amri Abeid, Arusha.

Mabao ya Simba yalifungwa na nahodha wa timu hiyo, John Bocco kwa mkwaju wa penalti dakika ya saba baada ya Bernard Morrison kuchezewa faulo ndani ya 18.

Bao hilo lilidumu mpaka dakika ya 59 ambapo Morrison alipachika bao la pili kipindi cha pili ndani ya 18 kwa pasi ya Clatous Chama.

Ushindi huo unaifanya Simba kutwaa taji la Ngao ya Jamii kwa kushinda mbele ya Namungo FC inayonolewa na Hitimana Thiery.
Share To:

msumbanews

Post A Comment: