Mamlaka 
 ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imevitoza faini ya Sh milioni 30 vyombo 
vya habari sita, kwa kukiuka kanuni na maadili ya utangazaji ikiwamo 
redio ya Clouds FM kuzungumzia supu ya pweza kuimarisha tendo la ndoa 
katika muda ambao wasikilizaji wanaweza kuwa watoto.
Mbali
 ya Clouds FM, vyombo vingine vilivyoadhibiwa ni East Africa Radio, na 
televisheni za Star, Sibuka, na Global Tv na Duma Tv.
Akisoma
 uamuzi huo jana jijini Dar es Salaam, Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya 
Maudhui ya TCRA, Joseph Mapunda alisema vyombo hivyo vilikiuka kanuni za
 mawasiliano kwa nyakati tofauti.
Mapunda
 alisema redio ya Clouds FM kupitia kipindi chake cha Jahazi, 
walihamasisha vitendo vya ngono, kwa kutumia supu ya pweza katika 
kuimarisha tendo la ndoa kwa muda ambao wasikilizaji wanaweza kuwa 
watoto.
Alisema
 baada ya kusikiliza utetezi wao, wanatozwa faini ya Sh milioni saba na 
kupewa onyo kali baada ya kuwatia hatiani kwa kosa hilo.
Katika
 shauri lingine, kituo cha Duma TV kimetozwa faini ya Sh milioni saba na
 kufungiwa kuchapisha maudhui kwa muda wa mwezi mmoja ili wajipange na 
kuzifahamu kanuni na kuzingatia weledi na maadili ya utangazaji.
Mapunda
 alisema Duma ilikutwa na hatia ya kukiuka kanuni kwa kuchapisha na 
kutangaza maudhui yenye lugha isiyo na staha na iliyo na udhalilishaji 
wa kijinsia kwa wanaume na wanawake.
Alisema
 redio ya East Africa imetozwa faini ya Sh milioni tatu na kupewa onyo 
kali kwa kukiuka kanuni hiyo, kwa kurusha maudhui ya kukashifu utendaji 
wa serikali kupitia uteuzi wa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za 
Serikali (CAG) na kutumia lugha ya kashfa dhidi ya utendaji wake.
Vilevile
 Global Tv imetozwa Sh milioni saba na kupewa onyo kali, baada ya 
kupatikana na hatia ya kuchapisha picha ya mnato na kutangaza maudhui 
yasiyokuwa na lugha ya staha na yenye kushabikia vitendo vya mahusiano 
ya kimapenzi ya jinsia moja.
Mapunda
 alisema maudhui hayo, yangeweza kuwaumiza na kuwakwaza waumini wa 
dhebebu la Anglikana na Watanzania kwa ujumla. Pia, alisema Sibuka Tv 
inatozwa faini ya Sh milioni tatu baada ya kupatikana na hatia ya 
kushabikia mauaji ya kutisha katika muda, ambao watoto wanaweza kuwa 
sehemu kubwa ya watazamaji.

Post A Comment: