mkurugenzi wa Star Intalinational Iringa Dkt Jesca Msambatavangu akizungumza na wanahabari mkoani Iringa (hawapo pichani) wakati akizindua mfumo wa ufundishaji wanafunzi wa shule za sekondari na msingi kupitia mitandao ya kijamii (online) wakiwa nyumbani kwa kujiunga kupitia Tovuti ya www.coronaseasonschool.com
..............................................
Na Francis Godwin, Iringa
Uongozi wa shule ya Star Intalinational Iringa umezindua mfumo mpya wa ufundishaji wa wanafunzi wa sekondari na shule za msingi nchini kwa njia ya mitandao ya kijamii (Online) ambapo wanafunzi watafundishwa wakiwa majumbani .
Akizungumza na wanahabari jana wakati akizindua mpango huo wa ufundishaji kwa njia ya mtandao mkurugenzi wa Star Intalinational Iringa Dkt Jesca Msambatavangu alisema kuwa mfumo huo utamwezesha mwanafunzi wa sekondari na yule wa shule za msingi kuweza kuendelea na masomo kama kawaida kwa wakati huu ambao shule zimefungwa .
" Kutokana na changamoto ya virusi vya Corona ambavyo vimeikumba dunia sisi kama wadau wa elimu tumeona kila mmoja kwa nafasi yake anapaswa kuangalia namna gani ya kuwasaidia watoto wa kitanzania ambao kwa sasa wanaendelea kukaa nyumbani pasipo kufundishwa "
Hivyo alisema kwa upande wa shule yake kutokana na changamoto hiyo alilazimika kubunia mbinu hiyo ya ufundishaji wanafunzi wake majumbani kwao kwa kuwapa kazi mbali mbali za kufanya na kusahishiwa kwa mtandao bila ya kukutana na mwalimu .
Alisema kupitia mfumo huo wa kimtandao wameweka utaratibu wa kila darasa ndani ya wiki kuweza kukutana na mwalimu kwa njia ya mtandao ambapo wanafunzi wataweza kufundishwa moja kwa moja (live) na kuweza kuuliza maswali mbali mbali ya kimasomo kutokanana kazi walizopewa .
Hata hivyo alisema mfumo huo wa ufundishaji utawalenga wanafunzi wote wa Tanzania wanaosoma sekondari na shule za msingi ambapo ili waweze kuendelea na masomo yao wakiwa nyumbani watatakiwa kujiunga na tovuti ya www.coronaseasonschool.com ama kupiga simu 0716 79 79 79 au 0653 797979.
Dkt Msambatavangu alisema kwa kupitia mfumo huo wa kimtandao wajibu wa mzazi utakuwa ni kuhakikisha wanawasimamia watoto wao kufanya kazi ambazo zinatolewa kupitia mtandao na kuzingatia vipindi .
Kwani alisema badala ya wazazi kuwaacha watoto wao wakitumia muda mwingi kucheza ama kutazama TV nyumbani ni vizuri sasa watoto hao wakazingatia muda wa masomo kwa kujiunga na mfumo huo rafiki kuweza kuendelea na masomo na kuwa masomo yamezingatia mitahala ya Tanzania .
Pia alisema anaendelea na mchakato na ikiwezekana basi mfumo huo kuuwezesha zaidi ili kufundisha masomo ya shule za Msingi na Sekondari kwa nchi zote za Afrika na kuwa wameamua kuweka gharama ndogo sana kwa wazazi wa kitanzania kwa ajili ya kujiunga na mfumo huo ili watoto wao kujisomea na kuwa hata kama shule zitafunguliwa bado mfumu huo hautafungwa utakuwa endelevu
Kwa upande wao baadhi ya wazazi mjini Iringa wamepongeza uzinduzi wa ufundishaji kwa njia ya mtandao na kuwa utasaidia watoto wao kuendelea kujisomea wakiwa nyumbani tofauti na ilivyo kuwa siku 30 za mwanzo baada ya serikali kufunga shule na watoto kukosa kufundishwa .
Tukuswiga Mwaisumbe alisema kuwa kupitia mfumo huo mzazi sasa atalazimika kujaza kifurushi kwenye simu janja ama kwenye Kompyuta ama Laptop ili kumwezesha mtoto wake kuweza kuendelea na masomo na kuomba uongozi wa shule hiyo kuja na kuhamishia mfumo huo kwenye radio za kijamii ili wananchi wa vijijini nao waweze kuwawezesha watoto wao kuendelea na masomo.
Huku Anani Ndelwa alisema kuwa kuanzishwa kwa mfumo wa masomo mtandaoni ni hatua kubwa na ya kujivunia kwa Tanzania kwani kupitia mfumo huo watoto wataweza kugeuka tabia na kuachana na matumizi ya mitandao ya kijamii kutazama katuni ama picha zisizo na maadili .
Post A Comment: