Na.Faustine Gimu Galafoni,Dodoma.
Kamati mbili [2]  za kudumu za Bunge zinawaalika wadau kutoa maoni yao kwa njia ya barua pepe kuhusu miswada mitatu [3] ya sheria  iliyosomwa bungeni kwa mara ya kwanza Februari,7,2020 wakati wa mkutano wa kumi na nane wa bunge.


Katika taarifa iliyotolewa na kitengo cha mawasiliano  na uhusiano wa kimataifa  Ofisi ya Bunge April 21,2020 ilitaja miswada hiyo kuwa ni pamoja na Muswaada wa sheria ya marekebisho ya  sheria mbalimbali  wa mwaka 2020 [The Written Laws[Miscellaneous Amendments ]Bill 2020  ulio chini ya Kamati ya kudumu ya katiba na sheria.

Wa pili ni  Muswada wa Sheria ya Afya ya mimea wa mwaka 2020 [The Plant  Health Bill ,2020]  chini ya kamati ya kudumu ya Bunge ya kilimo ,Mifugo na Maji.

Na Muswada wa tatu ni muswada wa sheria ya kusimamia na kuendeleza uvuvi wa mwaka ,2020 [The Deep Sea Fisheries  Management   and Development Bill ,2020] chini ya Kamati ya kudumu ya Bunge  ya kilimo, mifugo na Maji .

Kitengo hicho cha Mawasiliano na Uhusiano wa Kimataifa ,Ofisi ya Bunge katika taarifa yake ilifafanua kuwa Maoni kuhusu Miswada hiyo mitatu yatawasilishwa kwa katibu wa Bunge kwa njia ya barua pepe kamati@bunge.go.tz kabla ya tarehe 4 ,Mei,2020  na Miswada husika inaweza kupakuliwa  kupitia tovuti  WWW.Parliament.go.tz.

Share To:

msumbanews

Post A Comment: