Msanii Kenny Rogers (81) raia wa Marekani, amefariki Dunia akiwa nyumbani kwake.

Kwa mujibu wa familia yake kifo cha Msanii huyo ni cha kawaida na wala hakihusishwi na jambo lolote .

Rogers, alitamba kwa nyimbo zake nyingi zikiwemo The Gambler, Lady, Islands in the Stream na Lucille, huku akiwa ameuza rekodi zaidi ya Milioni na kushinda tuzo 3 za Grammy.

Kama muigizaji ametokea kwenye filamu ya Six Pack mwaka 1982 na katika tamthilia kadhaa maarufu za runinga kama The Gambler franchise, Christmas in America na Coward of the County.
Share To:

msumbanews

Post A Comment: