Mkuu wa mkoa wa Iringa Ally Hapi wa pili kushoto akimtazama mwanafunzi wa shule ya sekondari Mazombe aliyeanguka kwa njaa 
Wanafunzi wa sekondari ya Ibumu wakirejea nyumbani 
Mkuu wa mkoa wa Iringa Ally Hapi akipongezwa na wananchi wa Ibumu 

..........................
Na Francis Godwin, Iringa
BAADA  ya  wanafunzi  watatu  wa  shule  ya  sekondari Mazombe  wilaya ya  Kilolo  kuangua kwa  tatizo la  njaa  wakati wakimsikiliza mkuu  wa  mkoa wa  Iringa Ally Hapi  wakati wa ziara  yake ya Iringa  mpya  awamu ya pili ,mkuu  huyo wa  mkoa ameagiza  wazazi wote kuchangia chakula kwa  ajili  ya  watoto wao .

Akitoa  agizo hilo  mkuu    huyo  mkoa  alisema   kuwa  tatizo la  wanafunzi  kuanguka  kutokana na njaa  sio zuri  kwa  maendeleo ya elimu  katika  mkoa  wa Iringa ambao  unaongoza  kwa  uzalishaji wa mazao ya  chakula   hivyo  ni lazima  wazazi   wote  kuhakikisha  wanachangia  chakula  kwa ajili ya  watoto  wao ili  kila shule  uwepo  mpango wa  wanafunzi  kupata  chakula kwa  pamoja.

Kwani  alisema mazingira wanayotoka   wanafunzi hao yametofautiana na  wapo  ambao  wanatoka asubuhi  pasipo kula chakula  chochote  hivyo kushinda  shule  bila kula ni tatizo jingine  ambalo  linapelekea  mwanafunzi   kukosa  uwezo wa  kumsikiliza mwalimu .

“  Nimeshuhudia  leo  hata  wanafunzi  watatu wakianguka  kwa  kuishia  nguvu na baada ya  kuwauliza  wanasema hawajala  chochote  toka  walipokula chakula  usiku  wa jana  sasa  hili  si zuri  sana  mtoto anakuja  shule  bila hata kunywa  chai  na anashinda na njaa hadi anaanguka kwa  kuishia  nguvu  kutokana na njaa “ alisema mkuu  huyo  wa mkoa

Kuwa  lazima  kila  shule  kupitia kamati zake za  shule  kuweka utaratibu wa kuwahamasisha  wazazi   kuchangia chakula  ili  kuanzisha  utaratibu wa kula chakula shuleni  na  kuwa ambacho hataki  kusikia ni  wazazi  kuchangishwa  fedha za chakula .

“  Naagiza  wazazi  wote  kuanza kuchagia  chakula kwa ajili ya  watoto  wao wawapo  shule  na sitaki kusikia  wazazi  wakichangishwa  fedha za  chakula lazima  muweke  utaratibu wa kutengeneza bajeti ya chakula kwa  kila mwanafunzi anatakiwa  kuchangia mahindi na maharage  kiasi gani  ni  vitu  ambavyo kila mmoja anauwezo wa  kuchangia na sio  kulazimisha  wazazi kuchangia fedha  wengi  hawana uwezo wa  kutoa  fedha ila chakula  wanauwezo  huo “

Katika  hatua  nyingine  mkuu  huyo wa  mkoa  alieleza  kusikitishwa na kasi ya  wanafunzi kupata  mimba katika tarafa ya Mazombe   kutokana na miezi  miwili  pekee  wanafunzi 12   wa sekondari  kukatisha masomo  kutokana  na tatizo la mimba   hivyo  kuagiza wale  wote  wanaohusika na mimba   hizo  kusakwa na kuchukuliwa hatua za  kisheria.

Hapi  alisema  sehemu  kubwa sababu  zinazochangia wanafunzi hao  kupata  mimba ni kukaa nje ya  shule hivyo lazima  kuwepo mpango wa  shule  ambazo hazina   mabweni ya  wanafunzi  kuanzisha  ujenzi wa mabweni lakini  kuanzisha  utaratibu  wa  kuwalinda  watoto  wa kike  dhidi ya vijana  wanaojihusisha na mahusiano na  wanafunzi  hao .


Aidha  aliwataka  viongozi wa  tarafa ya mazombe  likiwemo  jeshi  la polisi  kufanya msako  kwa  wote wanaojihusisha kimapenzi na  wanafunzi hao pamoja  na  kuwakamata  wazazi  ambao wanamalizana na  watuhumiwa wa  mimba  za wanafunzi nje ya  vyombo  vya sheria.

Wakati  huo  huo Hapi  ameagiza  wanafunzi  wote  ambao  walichaguliwa  kujiunga na elimu ya  sekondari nab ado wapo  mitaani  kwa  kisingizio cha  kukosa  sare za  shule  kuripoti  shule  wakiwa na nguo  zao za  nyumbani .

Alisema kuwa walimu wasiwazuie  wanafunzi  wasio na  uwezo wa kununua  sare za  shule  kuripoti  shule  kuanza masomo kwani sare  haipaswi kuwa  kikwazo  cha watoto hao  kusoma   kuwa lengo la serikali ya  awamu ya tano  chini ya Rais Dkt  John Magufuli  kufuta  ada ni kutaka  watoto wote  wasome na gharama  kubwa   serikali inagharamia  elimu nchini  .

Hivyo  aliagiza  wazazi  ambao  watoto  wao  wamefaulu  na  hawapo shule  kukamatwa na  kufikishwa mbele ya  vyombo  vya sheria  kwani  kitendo cha mtoto  kulipiwa  gharama    na serikali kwa  ajili ya  kupata  elimu na mzazi  kushindwa  kumpeleka  mtoto  shule ni sawa na uhujumu uchumi .

Awali  mkuu wa  shule ya Sekondari Mazombe  Crispin Ngatunga   alisema  kuwa  kutokana na tatizo la  wanafunzi  kuanguka njaa uongozi wa shule  hiyo umekutana na  wazazi na kuweka mpango wa kuanzisha  utaratibu wa kuwapa chakula  shuleni hapo mpango ambao utaanza  wiki  hii .

Kuhusu mapokezi ya wanafunzi wa kidato cha kwanza  alisema kuwa  jumla ya  wanafunzi 251  walipangwa  katika  shule  hiyo kuanza masomo  mwaka   huu  walioripoti ni  wanafunzi 205 na  wanafunzi 26  hawajaripoti  hadi  sasa .
Share To:

Francis Godwin Mzee wa matukiodaima

Post A Comment: