Madiwani wa CHADEMA Halmashauri ya Jiji la Mbeya Ndg Lucas Mwampiki, Kata ya Mwakibete na Hussein Japhet Wasuha, Kata ya Itagano wametangaza kukihama chama hiko na kujiunga na CCM wakiungana na wenzao 11 waliojiunga awali. 

Kuhama kwa madiwani hao kunafanya idadi ya waliohama kutoka Chadema kwenda CCM kufikia 14 ambapo Januari 26 mwaka huu madiwani 11 wakiongozwa na aliyekuwa mstahiki meya Mchungaji David Mwashilindi walihamia CCM.

Kutokana na kuhama kwa madiwani hao hivi sasa CCM inakuwa na madiwani 17 huku Chadema ikiwa na madiwani 16 hivyo kuifanya Chadema kuipoteza Halmashauri ya Jiji la Mbeya.
Share To:

Post A Comment: