Na Englibert Kayombo, WAMJW – Moshi Kilimanjaro.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile amewaasa watumishi wa afya kutoshiriki kwenye makosa ya uhalifu kwa kuharibu ushahidi wa makosa ya jinai pindi wanapofanya uchunguzi wa kitaalam.

Dkt. Ndugulile ametoa kauli hiyo alipokuwa ziarani katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Kilimanjaro (Mawenzi) akizungumza na watumishi wa afya hospitalini hapo.

“Katika kosa ambalo hatutamsamehe mtumishi wa afya ni kushiriki katika uhalifu wa kuharibu ushahidi, hatutamvumilia mtu ambaye atashiriki kwenye makosa hayo” alisema Dkt. Ndugulile.

Alisema kuwa kesi za ukatili wa kijinsia mara nyingi huwa ni kesi za jinai huku wataalam wa afya wakipewa dhamana ya kuthibitisha ukweli wa matukio hayo na kuwataka kufuata miiko na maadili ya taaluma ya afya.

“Mtu amepata shambulio, daktari unasema kwamba huyu mtu hajashambuliwa, tumeshawahi kufanya hiyo na endapo tukithibitisha pasipo na shaka kwamba wewe mtaalam wetu umeenda kinyume na miiko na maadili ya kazi yako lazima tutakuchukulia hatua” alisisitiza Dkt. Ndugulile.

Mwisho
Share To:

msumbanews

Post A Comment: