Katibu mkuu wizara ya maliasili na utalii Prof Adolf Mkenda akifungua kikao cha tathimini ya maonesho ya utalii ya karibu kusini jana kilichojumuisha makatibu tawala wa mikoa yote ya nyanda za juu kusini leo ,kulia kwake ni mwenyekiti wa makatibu tawala Katibu tawala wa mkoa wa Iringa Happines Seneda 
Katibu mkuu wizara ya maliasili na utalii Prof Adolf Mkenda akionyesha jarida la kuelezea vivutio vya utalii kusini 
Mwenyekiti wa kamati ya Ma Ras ya utalii kusini ,Ras wa mkoa wa Iringa Happines  Seneda  akieleza faida ya maonesho  ya utalii ya karibu kusini 
 mkuu wa kitengo cha mawasiliano serikalini na msemaji wa wizara ya maliasili na utalii Dorine Makaya kulia kufuatilia kikao cha tathimini ya maonesho ya karibu kusini leo 
Baadhi ya wadau  wa utalii wakiwa katika kikao hicho 

Kamishina mwandamizi wa hifadhi za Taifa (TANAPA) kanda ya nyanda za juu kusini Dkt Christopher Timbuka kushoto akifuatilia kikao cha tathimini ya maonesho ya utalii ya karibu kusini leo  PICHA NA HABARI NA FRANCIS GODWIN 


WIZARA ya  maliasili na utalii  imesema  maonesho ya  utalii ya  karibu  kusini  yaliyofanyika mapema mwaka  huu mkoani Iringa kwa  ajili ya  kufungua lango la  utalii mikoa ya nyanda  za  juu  kusini   yameleta mafanikio makubwa kwa  wawekezaji mbali mbali  kutoka  ndani ya nchi na nje ya  nchi  kukusudia  kuja  nchini .

Akifungua  kikao  cha tathimini  cha maonesho  hayo  leo katika  ukumbi wa  chuo  kikuu  cha Elimu   Mkwawa  kikao kilichoshirikisha  makatibu tawala  wa  mikao yote ya nyanda za  juu kusini na  waalikwa  kutoka mkoa wa Mwanza ,katibu  mkuu  wa wizara ya maliasili na utalii Prof Adolf Mkenda  alisema  kuwa   kupitia maoneshi hayo   wizara  yake  imejipanga  kuona  inazitumia changamoto  zilizojitokeza  kuona  inaboresha  zaidi  maonesho  kama  hayo ambayo yanatarajiwa  kufanyika kanda ya  ziwa  .


"  Tathimini   hii inatupa   fursa  ya  kujifunza  changamoto  mbali mbali na mafanikio  yaliyotokana na maonesho  yaliyopita  na  wakati  mwingine  tunapoandaa maonesho kama  hayo  basi  kuweza  kutumia changamoto  hizo  kuboresha  zaidi  ili  kuweza  kuvutia idadi kubwa ya  wawekezaji na  kuona  Taifa  linapata  faida  kubwa  kutokana na  sekta  hii ya utalii nchini " alisema Prof Mkenda 

Kuwa uongozi  wa mkoa wa Iringa chini ya katibu tawala  wa mkoa  huo  Happiness Seneda  ambae  alikuwa ni  mwenyekiti wa maonesho ya karibu  kusini  waliweza  kufanya kazi kubwa ya  kuandaa maonesho hayo kwa  kushirikiana na makatibu  tawala wa  mikoa yote ya nyanda za juu kusini na hata  kuyafanya maonesho hayo kuliletea  heshima kubwa Taifa hasa katika  sekta ya utalii .


Alisema maonesho  kama hayo yamekuwa yakifanyika  hata  mwaka  juu  yalifanyika kwa mikoa   ya nyanda za  juu  kusini  ila ubora  wa maonesho ya safari  hii umetokana na makatibu tawala  wa mikoa ya nyanda za  juu  kusini  kwenda Kujifunza  kupitia  maonesho ya  utalii ya Kill Fair  ambayo  yamekuwa  yakiendesha  na sekta  binafsi na  kupitia ziara  hiyo ya mafunzo kwenye maonesho hayo  viongozi wa mikoa ya  nyanda  za juu kusini  waliweza  kutumia vizuri  ziara na kuboresha maonesho ya  karibu kusini .


Hivyo  alisema  kwa mwakani  kwenye maonesho kama  hayo  wanategemea  kuona  mambo mazuri  zaidi ya idadi ya  wawekezaji  inaongezeka   zaidi kwani  changamoto  chache zilizojitokeza  safari  hii  zitakuwa  zimepunguzwa ama  kumalizika kabisa .

Prof Mkenda alisema  lengo la wizara yake  ni kuona  fedha  za umma  zinatumika  vizuri na kuwa na mrejesho  mzuri  wenye  kuliletea Taifa faida na sio  kuliingizia  Taifa hasara  .


Alisema  katibu tawala wa mkoa wa Iringa kama  mwenyekiti wa maonesho ya karibu  kusini na timu yake  wameonyesha  umakini  mkubwa kwa  kufanya maonesho  mazuri kwa  gharama nafuu na fedha  zilizotengwa kwa ajili ya kazi hiyo  kutumika  na hata  kubaki akiba  jambo  mbalo  ni zuri  sana hasa katika  upande wa ubanaji matumizi katika  uendeshaji wa  shughuli mbali mbali .

" Niseme  tu  serikali inahitaji  kuona matokeo makubwa yanakuwepo kwa gharama nafuu na kuepuka  gharama na matumizi ya  fedha  yasiyo na ulazima katika kutangaza  utalii  nchini ndio maana  kuna mtumishi  wa  mmoja  wa  bodi ya Utalii Nchini (TTB) niliweza  kumsimamiasha kazi  jumapili  asubuhi baada ya  kutaka  kutoa  fedha  zaidi  ya  shilingi milioni 70  kwa ajili ya kutangaza  utalii kwa mtu  ambae hakuna  na mkataba  wowote na wizara  hatuwezi  kutumia  vibaya   fedha kwani matumizi yasiyofaa katika  wizara  hayaisaidii wizara kupiga hatua na sisi tunataka  kutumia   fedha zenye mrejesho  mzuri"  

Katika  hatua  nyingine  Prof  Mkenda  alisema kuwa kwa kuwa  serikali  imeamua  kuendeleza utalii nchini  wizara  yake  imejipanga  kuendeleza utalii kwa kufungua   milango ya  utalii katika kanda  zote za Tanzania tofauti na  ilivyokuwa awali  ambapo  nguvu   kubwa  ilielekezwa  hifadhi  za kaskazini pekee .

Aidha  alisema  kupitia  ukusanyaji wa mapato yatokanayo na sekta ya  utalii  kwa mara ya  kwanza  wameweza  kutoa gawio  la  zaidi ya bilioni 4 serikalini jambo mbalo  ni  la kujipongeza na  bado   wameendelea  kujipanga  kuendelea  kutoa gawio  kubwa  zaidi. 

Kwa  upande  wake   mwenyekiti wa makatibu tawala wa mikoa ya nyanda za  juu  kusini Happines  Seneda  alisema kuwa pamoja na maonesho hayo  kufana mwaka huu  wamejipanga  kuboresha  zaidi mwakani na kuwa changamoto  kubwa  zilizokuwepo  hasa   juu ya  Hoteli  za  wageni mkoa wa Iringa  umeanza  kutatua  changamoto  hiyo  kwa kugawa maeneo ya  ujenzi wa  Hoteli  zaidi za  kitalii na baadhi wameanza  kujenga  hoteli  za  kisasa ambazo awali  hazikuwepo .

Kamishina  mwandamizi  wa hifadhi za Taifa (TANAPA) kanada ya  kusini   Dkt  Christopher  Timbuka  alisema kuwa kupitia maonesha  ya karibu  kusini mwaka huu idadi ya  watalii na wawekezaji katika  hifadhi za  mikoa ya  kusini ikiwemo ya Ruaha  imezidi  kuongezeka  na  wapo  walioomba  kuwekeza katika ujenzi wa Hoteli .


Share To:

Francis Godwin Mzee wa matukiodaima

Post A Comment: