Abdul  Nondo kushoto akizungumza na wakili  wake Jebra Kambole ambae ni mmoja wa mawakili wa mtandao wa watetezi wa haki za binadamu Tanzania (THRDC) waliompigania kisheria 
           Na Francis Godwin,Iringa 

ALIYEKUWA mwenyekiti  mtandao wa Wanafunzi Tanzania (TSNP) Abdul Omary Nondo ambae  alikuwa  ameishinda jamhuri  katika  kesi  ya  kudaiwa  kujiteka na  kutuma taarifa  za  uongo  leo  ameshinda  tena  rufaa iliyokuwa  imekatwa na jamhuri  dhidi yake .

 Katika maamuzi hayo jamhuri imeshindwa kuithibitishia mahakama kuu kulingana na sababu za rufaa zilizoletwa na Jamhuri  huku mahakama kuu kanda ya Iringa imefikia kumwachia  huru  Nondo  baada  ya kujiridhisha kwamba upande wa serikali ulijielekeza vibaya kwa kukimbilia kufungua kesi dhidi ya mlalamikaji badala ya kushughulikia malalamiko yake kwa jeshi la polisi. 

Rufaa  ya  Nondo  imetolewa   hukumu na  jaji  wa mahakama  kuu  kanda ya  Iringa Panterine Kente ambapo  katika  maelrezo yake  wakati wa  kutoa   hukumu  hiyo  alisema hati ya maelezo (caution statement) iliyoletwa mahakamani haikuwa ushahidi tosha kwa jamhuri kwa kuwa ilikuwa na majina tofauti na majina  yaliyopo kwenye hati ya mashataka.

Kutokana na  hukumu  hiyo ya  kumwachia  huru  Nondo  sasa  anakuwa ni  raia   huru  katika nchi baada ya  hukumu  hiyo ya mahakama  .

Akizungumza  baada ya  kuachiwa  huru  kwa mara ya pili  sasa  Nondo  amemshukuru  Mungu  kwa  kusimama upande  wake  pia  amepongeza  watanzania  wote  ambao  walikuwa  wakimwombea  wakati  wote  pamoja na mtandao  wa watetezi wa haki  za  binadamu Tanzania (THRDC)  kwa  kumpigania hadi  mwisho .

 Nondo ambaye awali alishtakiwa katika mahakama ya wilaya Iringa alishtakiwa kwa kosa la kutoa taarifa za uongo kinyume na kifungu cha 16 cha Sheria ya Makosa Mtandaoni, 2015 ambapo aliushinda upande wa jamhuri kwakuwa Jamhuri ilishindwa kuthibitisha paspo shaka malalamiko waliyoleta mahakamani
Share To:

Francis Godwin Mzee wa matukiodaima

Post A Comment: