Na.Faustine Gimu Galafoni,Dodoma.

Rais wa Jamhuri ya Muungano Wa Tanzania Mhe.John Pombe Magufuli amewataka watanzania kuepuka  kuwasikiliza vibaraka wa ndani ya nchi wanaotumiwa na Mabeberu kutoka Mataifa ya nje kuharibu sifa njema  ya
Taifa la Tanzania.

Rais Magufuli ameyasema hayo leo Nov.21,2019  katika mahafali ya  chuo kikuu cha Dodoma yaliyokwenda sambamba na zoezi la Kutunukiwa  Shahada ya heshima ya udaktari  Falsafa ambapo amesema kwenye Mafanikio na Changamoto zipo ,hivyo amebainisha  hatokatishwa tamaa na Mabeberu huku akiwataka watanzania kuwa na mshikamano  na  Uzalendo  kwa Maendeleo Taifa .

Rais Dokt.Magufuli amesema Tanzania ina vivutio vingi ambapo duniani kote Nchi ya Tanzania ni ya Pili kwa vivutio vya utalii na ni nchi ya pekee Duniani yenye Madini ya Tanzanite hivyo amewataka watanzania Kuacha kulalamika kwani Tanzania ni tajiri na kinachotakiwa ni kufanya kazi kwa bidii.

Aidha,Rais  Dokta.Magufuli amesema Uchumi wa Tanzania Unaendelea kuimarika ukikua kwa asilimia saba[7}na kuifanya Tanzania kuwa miongoni mwa nchi tano zinazokua kiuchumi kwa kasi miongoni mwa nchi
Tano{5]barani Afrika.

Rais Magufuli ni wa tatu kutunukiwa Shahada ya  heshima ya Udaktari wa Falsafa [ Honorary PhD] , ambapo wa kwanza ni aliyekuwa Waziri Mkuu miaka ya 1962 hadi 1977  Hayati Rashid Mfaume Kawawa akifuatiwa na
Rais  Mstaafu wa awamu ya nne Jakaya Mrisho Kikwete .

Share To:

msumbanews

Post A Comment: